
Na Boniface Wambura, Dar es salaaam
Imechapishwa Mei 26, 2014, saa 9:55 alasiri
Tanzania
imeendelea kung’ang’ara kwenye Michezo ya Afrika kwa Vijana (AYG) kwa upande wa
mpira wa miguu kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 baada ya jana (Mei 25
mwaka huu) kuichapa Swaziland mabao 3-0.
Mabao
ya Tanzania katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa jijini Gaborone,
Botswana yalifungwa na Amani Ally dakika ya sita, Nasson Chanuka dakika ya 32
wakati Amos Kennedy alikamilisha ushindi huo kwa bao la dakika ya 53.
Katika
mechi yake ya kwanza, Tanzania ilitoka sare ya bao 1-1 na Mali na baadaye
kuwafunga wenyeji Botswana mabao 2-0. Mechi za michuano hiyo zinaoneshwa moja
kwa moja na kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini.
Tanzania
itacheza mechi yake ya nne kesho (Mei 27 mwaka huu) dhidi ya Nigeria wakati
mechi ya mwisho itafanyika Mei 29 mwaka huu dhidi ya Afrika Kusini.
0 comments:
Post a Comment