![]() |
Sunday Kayuni atakuwa moya ya wakufunzi wa kozi hiyo |
Imechapishwa Mei 26, 2014, saa 10:00 jioni
Na Boniface Wambura, Dar es salaam
Kocha a ukocha wa mpira wa miguu
kwa ajili ya Leseni A na B zinazotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu
Afrika (CAF) zitafanyika jijini Dar es Salaam
kuanzia Juni 2 mwaka huu.
Ada
kwa kozi ya Leseni A itakayoanza Julai 21 hadi 26 mwaka huu ni sh. 300,000
wakati ile ya Leseni B itakayofanyika kuanzia Juni 2 hadi 15 mwaka huu ni sh.
200,000. Maombi ya kushiriki kozi hizo yatumwe kwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakati kwa upande wa Zanzibar yatumwe kwa Katibu
Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kabla ya Mei 31 mwaka huu.
Washiriki
ambao watajitegemea kwa chakula watalipa ada hizo wakati wa usajili
utakaofanyika Juni 1 mwaka huu kwa upande wa Leseni B na Leseni A watalipa
Julai 20 mwaka huu vilevile wakati wa usajili.
TFF
itatoa malazi kwa washiriki kwenye hoteli yake iliyopo Uwanja wa Kumbukumbu ya
Karume wakati wakufunzi wa kozi hizo ni Sunday Kayuni na Salum Madadi ambao wanatambuliwa
na CAF. Pia CAF baadaye itatuma Mkufunzi atakayetunga na kusimamia mitihani
hiyo.
0 comments:
Post a Comment