Mabondia
Mbwana Matumla wa Tanzania na David Charanga kutoka nchini Kenya wamepima uzito
maeneo ya sinza leo jijini Dar es salaam kuelekea katika pambano lao la kukata
na shoka litakalofanyika kesho uwanja wa taifa wa burudani Ukumbi wa Dar Live Mbagala ikiwa ni sehemu ya kusherekea
sikukuu ya Krismas.
MBWANA MATUMLA |
Rais
wa oganaizesheni ya ngumi za kulipwa Tanzania TPBO Yasin Abdalaah Ustadhi
amesema mabondi wote wana uzito sahihi kwani Matumla ana kilo 57 na mwenzake
Charanga ana kilo 57 ,hivyo pambano lipo tayari .
Yasin
amewataka mashabiki wa ngumi kujitokeza kwa wingi hapo kesho katika ukumbi wa
Dar Live kushuhudia mabondia hao bora wa afrika mashairiki watakapo panda
ulingoni kurushiana masumbwi.
0 comments:
Post a Comment