
Kauli hiyo ilitolewa waziri huyo
jijini Dar es Salaam leo, wakati alipofanya ya ziara ya kushtukiza
kwenye Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi majira ya saa
11:30 alfajiri, ili kujionea utendaji kazi wa Mamlaka ya Udhibiti
Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), na Kikosi cha Usalama
Barabarni (Trafic), haswa katika udhibiti wa nauli holela katika kipindi
hiki cha sikukuu ya Chrismas na mwaka mpya.
Alisema uwamuzi wake huo
unatokana na kubaini kuwa Halmashauri hizo, zimekuwa zikiwalazimisha
madereva kuingiza magari (Mabasi), kwenye vituo hivyo ambavyo siyo
rasmi kwa lengo la kujikusanyia ushuru.
Amevitaja vituo hivyo vilivyolalamikiwa kwa usumbufu huo, kuwa ni pamoja na Mafinga, Kibaigwa, Nzega, Kibaha na vingine.
“Madereva wamekuwa
wakilazimishwa kuingia katika stendi hizi hata kama hawana abiria
wakushuka amakupakia, kitendo ambacho kinawapotezea abiria muda wao
wakufika kule wanakokwenda bila sababu za msingi”alisema Dk Mwakyembe.
Alisema utaratibu huo
haukubaliki, endapo ukiachwa uendelee hivyo iko siku watazuka watu
watafikia hatua ya kuanzisha vizuizi kama hivyo majumbani mwao lengo
likiwa ni kuibia wananchi.
Dk Mwakyembe amezitaka Halmashauri hizo kuacha utaratibu huo na baadala yake watafute vyanzo vingine vya ukusanyaji mapato.
0 comments:
Post a Comment