![]() |
Nadir Haroub 'Cannavaro' |
Ukiwafuatilia makocha wengi Duniani, hupendelea kuwafundisha
wachezaji kupiga penalti upande wa pembeni wa goli kuliko katikati.
Mpira ukipigwa pembeni ya goli una asilimia kubwa ya kuingia
kwasababu ya kasi au Golikipa kuchelewa kufika, lakini katikati ni kama
kuchezea shilingi chooni.
Kwa vile wachezaji wengine wana kiburi kutokana na uzoefu wao
pamoja na utaalam, haamua kuleta vionjo katika upigaji wa penalti ingawa utundu
huu unaweza kumfanya Shujaa au ziro kabisa.
Moja ya wanasoka wenye kiburi cha kupiga penalti za vionjo
ni kiungo wa zamani wa Juventus, Andrea Pirlo ambaye hupendelea kupiga penalti
aina ya panenka.
Aina hii ya penalti hupigwa katikati ya goli na kipa huhama
upande wa kulia au kushoto, huku mpira ukipita katikati kwa juu. Panenka ni
penalti ambayo inakuweka katikati ya ushujaa na u-ziro.
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' aliwahi kupiga
panenka dhidi ya Al Ahly ya Misiri katika mechi ya ligi ya mabingwa barani
Afrika iliyopigwa mjini Alexandria, Misri, Yanga wakitolewa kwa matuta.
Cannavaro alionekana shujaa, alishangiliwa mno, lakini jana
amejaribu kupiga panenka dhidi ya Gor Mahia na kuchemsha.
Makocha wanasemaje kuhusu Panenka?
"Penati ya namna ile wanaita Panenka ambayo unaweza
kuwa shujaa au ziro, ukifunga wewe ni shujaa, ukikosa watu wanakuona wewe ziro.
Nadir Haroub 'Cannavaro' anatakiwa
kubeba lawama, timu imepata penalti dakika za mwisho na inatakiwa kusawazisha
kwenye mechi ya kwanza na muhimu ya
kombe la Kagame, yeye akaamua kupiga penalti ya Panenka. Angefunga angeonekana shujaa. Ukipiga panenka inatakiwa
golikipa ahame kutoka kulia kwenda kushoto, lakini kipa wa Gor Mahia kwa bahati
mbaya hakuhama, Nadri Haroub anatakiwa kukubali lawama". Amesema mchezaji
wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Ally Mayay Tembele.
Makocha hufundisha kupiga penalti ya Panenka?
"Hakuna mwalimu yeyote anayeweza kuridhia au
kumfundisha mchezaji kupiga penalti ya namna ile, walimu wote Duniani nikiwemo
mimi nafundisha kupiga penalti pembeni, ndiko kuna asilimia nyingi za kufunga
kutokana na kasi ya mpira au golikipa kuchelewa kufika. Penalti za katikati ya
goli ni uwezekano tu, ni sawa na kuchezea shilingi chooni". Amefafanua
Ally Mayay.
0 comments:
Post a Comment