Sunday, July 19, 2015

UWANJA wa Taifa jijini Dar es salaam jana ulilipuka kwa Shangwe  nyingi baada ya mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma kufunga goli la kuongoza mapema dakika ya nne, Yanga ikifa 2-1 dhidi ya Gor Mahia katika mechi ya ufunguzi ya Kombe la Kagame.
Mashabiki waliovalia jezi za rangi ya kijani na njano walimtukuza Ngoma ambaye amekuwa mkali wa kufunga tangu atue Jangwani siku za karibuni kutokea FC Platinum ya Zimbabwe.
Lakini furaha hiyo ilizimika baada ya Ngoma kupewa kadi nyekundu kipindi hicho hicho cha kwanza baada ya kumfanyia 'uhuni'  mchezaji wa Gor Mahia.
Hivi kadi nyekundu aliyopata Ngoma alistahili akiwa ni mchezaji wa kulipwa?
"Hapana shaka kiwango cha Donald Ngoma kwa mechi ambazo nimemuona, ni mshambuliaji ambaye anaweza kutegemewa kutokana na urefu wake, uwezo wa kukaa na mpira, ana sifa za kufunga kwa kuibia na hata kwa kutumia nguvu kutokana na umbile.".

"Bahati mbaya sana  hana 'Proffesional Altitude' ambayo ni kuwa makini, unajua unapokuwa mchezaji mahiri na bora, unatakiwa kuwa makini na watu wanaokukaba na kuweza kuzuia hasira.  Kwa kadi nyekundu aliyopewa (Ngoma) inaonekana ni mtu ambaye matukio yake yanaweza kuigharimu timu. Kadi ya kwanza ya njano haikustahili kwa Proffesional Player kwasababu beki alikwenda kuchukua mpira akamvuta mkono, lakini kadi ya pili mchezaji akawa kama amemkanyaga akamvuta mkono. Kama mchezaji Proffesional anatakiwa kujiupusha na matukio hayo, analipwa fedha nyingi, tena ametoka mbali huko Zimbabwe". Amesema mchezaji wa zamani wa Yanga na Taifa Stars ambaye kwasasa ni kocha na mchambuzi wa soka nchini, Ally Mayay Tembele.a

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video