Mlinzi na kiungo wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Ally Mayay Tembele (wa pili kushoto) akitazama mechi ya Yanga dhidi ya Gor Mahia jana uwanja wa Taifa.
MOJA ya stori kubwa hapa mjini ni Mabingwa wa Tanzania bara,
Young Africans kuchapwa magoli 2-1 na
Gor Mahia ya Kenya katika mechi ya ufunguzi ya kombe la Kagame iliyopigwa jana
uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Mashabiki wengi wa Yanga wameonekana kutokuwa na hofu hasa
wakirudisha kumbukumbu zao nyuma ambapo walianza kwa kipigo, lakini wakamaliza mashujaa kwa kutwaa
ubingwa.
Takwimu haziongopi na kuna wakati zinajirudia, ingawa katika
mpira huu wa kisayansi zinaweza kubaki kwenye makaratasi tu.
Mwaka 1993, Wenyeji
wa Kombe la Kagame wakiwa Uganda, mechi ya kwanza Yanga ilifumuliwa 3-1 na
wenyeji SC Villa 'Jogoo', lakini walipokutana fainali Wanajangwani wakatoa
risasi 2 - 1 na ndoo ikatua Jangwani.
Rekodi inayofanana na hiyo ikajirudia tena mwaka 1999,
Wenyeji wa Kagame wakiwa wale wale Uganda.
Kipute cha kwanza Yanga ilifungwa na Rayon Sports ya Rwanda mabao 3 - 0,
ikaingia fainali na SC Villa na kushinda kwa penati, shujaa akiwa ni Peter
Manyika Sr.
Moja ya wachezaji waliokuwepo katika kikosi cha Yanga 1999
ni Ally Mayay Tembele ambaye amefanya mahojiano maalum na mtandao huu na kutoa simulizi hii ya kusisimua.
Swali: Mwaka 1999 Yanga ilianza kwa kufungwa kombe la Kagame
lililofanyika nchini Uganda na wewe ukionesshwa kadi nyekundu kama ilivyotokea
kwa Donaldo Ngoma jana uwanja wa Taifa, lakini mkachukua ubingwa, tueleze
mazingira ya kadi nyekundu uliyopata......
Ally Mayay: Hii ilikuwa mechi yangu ya kwanza ya kimataifa
kuichezea Yanga, mpira ukawa unaingia golini, nikauzuia kwa mkono, nikapewa
kadi nyekundu ya moja kwa moja pamoja na penalti, kiukweli walifunga wale Rayon
Sports, ilikuwa mechi ya ufunguzi.
Swali: Said Mwamba Kizota alikuwa anacheza namba tisa na
baada ya wewe kuoneshwa kadi nyekundu akarudi kucheza mkoba (mlinzi wa kati),
hebu tukumbushe tukio hilo....
Ally Mayay: Kweli Said
Mwamba alikuwa namba 9, baada ya mimi kupewa kadi nyekundu ikabidi arudi
kucheza nafasi ya beki wa kati . Baada ya mechi ile, mechi zote zilizofuata
tulishinda. Tukaingia fainali na SC Villa, tukatoka droo ya moja moja ndani ya
dakika 120 pale Nakivubo, tukaenda kupiga penalti, tukashinda na mimi ndiye nilikwenda kupiga
penalti ya mwisho ya kuchukua ubingwa .
Swali: Viongozi na makocha waliwaambia nini baada ya
kufungwa mechi ya kwanza na kadi nyekundu juu?
Ally Mayay: Baada ya kupewa kadi nyekundu mechi ya kwanza
tulikumbushwa na mwalimu Shungu pamoja na akina Said Mwamba Kizota kwamba 1993 walianza kwa kufungwa goli 3, lakini
walikwenda mpaka wakachukua ubingwa.
Nasisi tukataka kuonyesha historia waliyoonesha mwaka 1993,
walitupa moyo kwamba 1993 nao walipewa
kadi nyekundu, wakachukua ubingwa. Tukasema
kadi nyekundu isituvunje moyo, mechi zilizofuata tulicheza vizuri, mimi
nilikosa mechi iliyofuata tu, lakini nyingine zote mwalimu aliendelea
kunipanga.
Swali: Mechi ya fainali dhidi ya Sports Club Villa, Said
Mwamba Kizota alipewa kadi nyekundu, ilikuwaje mkapambana mpaka mwisho mkiwa
pungufu?
Ally Mayay: Mechi ya fainali nakumbuka alipewa kadi nyekundu
Said Nassor Mwamba Kizoto, tukacheza pungufu, lakini tulikuwa pungufu kwa
dakika chache, tulifanikiwa kuwabana Villa mpaka dakika 120 na tukachukua
ubingwa kwa Penalti.
Swali: Unaionaje nafasi ya Yanga kutwaa ubingwa mwaka huu?
Ally Mayay: Nafasi bado ipo kwa Yanga, lakini mechi ya KMKM
na Telecom ya Djbout sio ya kudharau. Bado Yanga wanaweza kufanya vizuri kama
wataambiwa kwamba huko nyuma waliwahi kuanza kwa kupoteza na wakachukua
ubingwa.
Kumbukumbu nyingine zinaonesha kwamba 2011, Tanzania wakiwa
wenyeji wa kombe la Kagame, Yanga walitoka sare ya 2-2, fainali wakaingia na
Simba na kuwafunga goli 1 - 0, bao la Kenneth Asamoah aliyemalizia krosi ya
Kigi Makassy.
Mwaka 2012 Tanzania wakiwa wenyeji kwa mwaka wa pili
mfululizo, mechi ya kwanza Yanga ikapigwa 2 - 0 na Atletico ya Burundi, fainali
wakaingia na Azam FC na kuwachapa mabao 2 - 0. Magoli ya Hamis Kiiza na
Said Bahanuzi.
Mwaka huu wameanza kwa kichapo, swali ni je, Historia
inaweza kujirudia?
0 comments:
Post a Comment