Monday, May 4, 2015


WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamefikisha pointi 44 katika nafasi ya tatu baada ya kucheza mechi 25, pointi moja nyuma ya Azam fc waliopo nafasi ya pili kufuatia kushuka dimbani mara 24.
Magoli ya Ibrahim Hajib dakika ya 48 na Ramadhan Singano dakika ya 64 yalitosha kuwapa Simba dhidi ya Azam fc katika mechi ya ligi kuu iliyopigwa jana uwanja wa Taifa. Goli la Azam lilifungwa na kiungo Mudathir Yahya dakika ya 58.
Ili Simba wachukue nafasi ya pili wanahitaji kushinda mechi ya mei 9 dhidi ya JKT Ruvu uwanja wa Taifa, halafu Azam wafungwe na Yanga kesho kutwa  na kutoa sare mechi ya mwisho dhidi ya Mgambo JKT.
Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic baada ya kufanikiwa kuzifunga timu mbili za juu msimu huu, Yanga na Azam, amesema sasa swali la timu gani bora nchini limeshajibiwa.

“Niliiandaa vizuri timu yangu, Azam fc ni mabingwa na bado nawaona ni mabingwa, ni timu ngumu, nina furaha sana kwasababu nilikuwa na msongo wa mawazo, sio mimi tu, kila mtu ndani ya timu’. Amesema Kopunovic na kuongeza: “Nina furaha sana, najivunia sana kuwa timu yangu ndio bora nchini Tanzania, tulimfunga Yanga, tumemfunga Azam, nadhani hakuna swali tena ni timu gani bora Tanzania”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video