Monday, May 4, 2015

YANGA SC wameshangazwa na kitendo cha mahasimu wao Simba kuwabeza kwa matokeo waliyopata katika mechi mbili za hatua ya 16 ya kombe la Shirikisho dhidi ya Etoile du Sahel.
Mabingwa hao wapya wa Tanzania bara walitoka sare ya 1-1 uwanja wa Taifa majuma mawili yaliyopita na juzi walifungwa 1-0 na Etoile, hivyo kutolewa kwa ushindi wa jumla ya magoli 2-1.
Mkuu wa Idara ya mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro amesema: “Wenzetu wa upande wa pili (Simba) wanatubeza kwa matokeo tuliyopata, sisi hatuna kinyongo na matokeo hayo, timu ilicheza kwa kiwango cha juu. Angalia kipindi cha pili hali ya umiliki wa mpira sisi tulikuwa na asilimia 51 kwa 49 za Etoile du Sahel, sasa anaanzaje kubeza kiwango chetu”
“Wao waache watubeze tu, lakini sisi ni wa kimataifa zaidi, tunakuja nyumbani kumalizia mechi zetu mbili za ligi kuu kwa ubora uleule, tukimaliza tutawapumzisha vijana wetu mahiri na mwakani wakimataifa watarudi tena kwenye ligi ya mabingwa”.

Yanga itacheza mechi ya ligi kuu kesho kutwa dhidi ya Azam fc kabla ya kusafiri kwenda Mtwara kuchuana na Ndanda fc mei 9 mwaka huu.
Msafara wa Yanga unatarajia kutoa leo uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Dar es salaam majira ya saa 8:00 mchana.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video