Wednesday, May 27, 2015

Hawa sio vijana wa mitaani, ni timu ya Taifa

TIMU ya Taifa ya masumbwi inayojiandaa kwa ajili ya michuano ya ‘All African Games’ na michuano mingine ya klabu bingwa ya Taifa inaendelea na mazoezi yake kwenye viwanja vya nje ya uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kitu cha kusikitisha ni mazingira ambayo timu hiyo inajiandaa, wachezaji wanafanya mazoezi chini ya mti eneo ambalo pia halina sakafu (kwenye mavumbi),  pia eneo hilo ni la wazi kitu ambacho ni hatari kwa afya zao.

Kocha wa timu hiyo Jonas Mwakipesile amesema anasikitishwa na hali hiyo na kuongeza kuwa inakatisha sana tamaa kuanzia wachezaji mpaka walimu kwa ujumla.

“Kama unavyoona mwenyewe, hawa ni vijana wa timu ya Taifa ya masumbwi wanafanya mazoezi nje, kwenye mavumbi, lakini wakiwa hawana vifaa vya mazoezi kama vile gloves, jezi na viatu. Kuna gloves chache ambazo hazitoshi wachezaji wote lakini pia sio za timu, tumeazima kwenye timu ya jeshi (JKT)”, amesema Mwakipesile.


“Timu haina kambi, kila mchezaji anatoka kwao na hatujui kama wachezaji wanakula vizuri kama inavyotakiwa, hawapati posho wala kifuta jasho, wanajitolea tu. Maana hawa wanajiandaa kupambana na mabondia wengine wa Afrika, inasikitisha na inakatisha tamaa. Kwa mwendo huu unatarajia mchezaji atakuwa na moyo wa kupambana wakati haoni ‘support’ yoyote?”, Mwakipesile alihoji.

“Lakini pale timu inapofanya vibaya tumekuwa tukinyooshewa vidole na watanzania wote, lakini wao hawajui haya yote yanayoendelea, laiti kama wangekuwa wanajua wangezuia hata timu isiende kwenye mashindano”, aliongeza Mwakipesile.

“Chakushangaza timu nyingine za Taifa zinapewa kila kitu kinachohitajika lakini hazifanyi vizuri, kwa mfano Taifa Stars inapewa karibu kila kitu lakini bado ina matokeo mabovu. Inasafiri kwa ndege, inawekwa kambini, inapata vifaa vya michezo lakini hatujaona matokeo mazuri,” amesema.

Kocha huyo amesema kuwa, wamejaribu kuomba kutumia eneo la uwanja wa Taifa lenye sakafu lakini wakaambiwa wakaombe kwenye wizara husika maana ndiyo yenye dhamana ya uwanja huo.

Kocha Jonas Mwakipesile

Mwakipesile kupitia mtandao huu  ameiomba serikali, wapenzi na wadau wa mchezo wa masumbwi kuangalia uwezekano wa kuboresha mazingira ya kikosi hicho na sio kusubiri kutoa lawama pale timu inapofanya vibaya kwenye mashindano.



Timu hiyo inatarajia kwenda kucheza michezo ya kirafiki nchini Zambia kwa ajili ya kujipima kabla haijasafiri kuelekea nchini Congo Brazzaville ambako michuano hiyo itafanyikia.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video