Saturday, February 14, 2015

Leo watashingilia kama hivi?

MABINGWA mara 24 wa Tanzania, Dar Young Africans wanashuka dimba la Taifa leo kucheza mechi ya kwanza ya raundi ya awali ya kombe la Shirikisho dhidi ya klabu ya jeshi ya BDF XI ya Botswana.

Hii ni mechi muhimu kwa Yanga kama wanataka kusonga mbele hatua inayofuata.

Waswahili husema ‘Mcheza kwao hutunzwa”. Uwanja wa nyumbani ni sehemu pekee ya kutengeneza matokeo ingawa kwa mpira wa kisayansi tulionao sasa, Mgeni anaweza kukufunga hata ukiwa nyumbani kwako.

Hata tunaposhuhudia michuano mikubwa kama UEFA, timu za ulaya zinajitahidi kutumia vizuri nafasi ya nyumbani kupata matokeo, ingawa nyingine hufungwa nyumbani na ugenini.

Uwanja wenu, mashabiki wenu, wanalala kwenu, wanakula vyakula vyenu, kwanini BDF wawafunge?

Timu hii ni mahiri sana kule Botswana, lakini kwa ubora waliokuwa nao Yanga, bila shaka watakalishwa.

Siku za karibuni Yanga wamekuwa na tatizo la kutumia nafasi wanazopata uwanjani katika mechi za ligi. Timu ina washambuliaji hatari kama Kpah Sherman, Amissi Tambwe, Simon Msuva, Danny Mrwanda, Mrisho Ngassa na wengineo.

Lakini ni kawaida kwa Yanga kupata nafasi tano wakafunga moja au wasifunge kabisa. Hata kocha Hans van der Pluijm amekiri kuwepo kwa tatizo la umaliziaji.

Michuano ya Shirikisho ni mikubwa barani Afrika, timu zinazoshiriki ni kubwa pia. Yanga wakumbuke wanaenda kucheza na timu nzuri ya Botswana. Hawa ni makamu bingwa kama ilivyo kwao Yanga Tanzania.

Cha msingi ni kuhakikisha wanacheza kwa nidhamu ya hali ya juu na kutumia kila nafasi watakayopata ili kupata ushindi mkubwa.

Ushindi wa kuanzia mabao 3-0 utakuwa na faida kubwa kwa Yanga kwani itakuwa rahisi kwao kulinda ugenini kwa maana ya Wapinzani wao watahitaji mabao 4-0 ili kuwatoa Yanga.

Lakini ushindi wa bao 1-0 au 2-0, 2-1, 3-2 utawaweka Yanga mazingira magumu kwani lolote linaweza kutokea ugenini, hata kama wanaweza kulinda  ushindi wa goli 1-0 ugenini.

Mashabiki wa Yanga jitokezeni kwa wingi, wale wa mikoani iombeeni dua timu yenu hata kama imewanyima haki ya kuuona mchezo huo kupitia Televisheni.


Kila la kheria Dar Young Africas katika mechi yenu ya leo!!.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video