Saturday, February 14, 2015

DSC_0023
LIGI kuu Tanzania bara inaendelea leo kwa mechi tatu kupigwa katika miji mitatu nchini.

Mechi inayovuta hisia za mashabiki wengi ni ile ya Tanga inayowakutanisha Wagosi wa Kaya, Coastal Union dhidi ya Mbeya City fc.

Msimu uliopita, Coastal waliifunga Mbeya City fc mabao 2-0 katika uwanja huo, hivyo Wagonga nyundo hao wa Nyanda za juu kusini wanataka kufuta uteja.

Katika msimamo wa ligi, Coastal wapo nafasi ya 7 wakijikusanyia pointi 18 baada ya kushuka dimbani mara 14.

Mbeya City wapo nafasi ya 10 wakiwa na pointi 16 kibindoni baada ya kucheza mechi 13.

Timu yoyote itakayopata ushindi itapanda nafasi kadhaa katika msimamo ukizingatia hakuna utofauti kubwa wa pointi kwa timu zote mpaka sasa.

Mechi nyingine za leo ni baina ya Ndanda fc na Mtibwa Sugar uwanja wa CCM Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara, wakati Stand United ipo uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga kuchuana na Mgambo Shootings.


Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mechi mbili, Polisi Morogoro wataikaribisha Simba uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro, wakati Kagera Sugar watachuana na JKT Ruvu  Kambarage, Shinyanga.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video