Monday, February 16, 2015

SHIRIKISHO la soka Tanzania, TFF, limefanyia marekebisho ratiba ya ligi kuu Tanzania bara sambamba na mechi za viporo.

Kwa mujibu wa ratiba mpya iliyotumwa kwa vyombo vya habari leo, alhamisi ya wiki hii (februari 19 mwaka huu)  kutakuwa na mechi mbili za viporo.

Tanzania Prisons watachuana na Yanga katika mechi ya kiporo uwanja wa CCM Sokoine, Mbeya, wakati Azam fc wataikaribisha Ruvu Shootings ya Pwani katika uwanja wake wa nyumbani wa Azam Complex.

Mwishoni mwa wiki hii, jumamosi ya februari 21 na jumapili februari 22 mwaka huu mechi kadhaa zitapigwa viwanja mbalimbali.

Jumamosi, Kagera Sugar watachuana na Polisi Morogoro uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga, wakati Ndanda fc watamenyana na Coastal Union dimba la Nangwanda Sijaona, Mtwara.

Mgambo JKT itapepetana na Mtibwa Sugar uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga.

Jumapili; Stand United watatifuana na Simba uwanja wa Kambarage, wakati Azam fc watashuka dimbani dhidi ya Tanzania Prisons, mechi hii itapigwa usiku uwanja wa Azam Complex, Chamazi.

Yanga ya Dar es Salaam itashuka dimbani ugenini kukabiliana na Mbeya City katika uwanja wa Sokoine.

MECHI ZA VIPORO

Februari 22, 2014, Mbeya City fc v Yanga, uwanja wa Sokoine

Machi 18, 2015, Mtibwa Sugar v Tanzania Prisons , uwanja wa Manungu.


Tutaendelea kukujuza ratiba nzima kadri mechi zinavyochezwa….

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video