Saturday, September 6, 2014

Mbwana Samatta (kushoto) na Thomas Ulimwengu (kulia) wataionesha kazi Burundi iliyoitungua 3-0 Taifa Stars Aprili 26 mwaka huu uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam


TIMU ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars inaendelea kujinoa katika mazoezi yake ya mwisho mwisho mjini Bujumbura kuelekea kuchuana na Burundi hapo kesho (septemba 7 mwaka huu).

Mechi hiyo ya kimataifa ya kirafiki ipo katika kalenda ya Shirikisho la soka Duniani, FIFA.

Kikosi cha wa wachezaji 20 wa Stars tayari kilishatua Bujumbura tangu jana na tayari kilishaanza kuzoea hali ya hewa nchini humo, huku morali ya wanandinga wote ikiwa juu kabisa.

Stars itaongozwa na Watanzania wawili wanaokipiga TP Mazembe ya DR Congo, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu kulipa kisasi cha kufungwa mabao 3-0 na Burundi katika mchezo maalumu wa kirafiki uliofanyika April 26 mwaka huu uwanja wa Taifa kuadhimisha miaka 50 ya Muungano.

Katika mechi hiyo kikosi cha Stars iliyosheheni wachezaji waliotoka katika mpango maalumu wa maboresho ya Taifa Stars uliofanywa na shirikisho la soka Tanzania, TFF,  ilishindwa kuhimili makali ya washambuliaji wa Burundi kama vile Didier Kavumbagu na Amiss Tambwe, lakini kesho itaingia kikosi kamili gado.

Wachezaji waliopo Burundi chini ya kocha Mholanzi, Mart Nooij ni makipa Mwadini Ali (Azam fc) na Deogratius Munishi ‘Dida’, (Yanga).

Wachezaji wengine ni Shomari Kapombe (Azam fc), Oscar Joshua (Yanga), Said Mourad (Azam fc), Nadir Haroub ‘Cannavaro’ (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga), Joram Mgeveke (Simba).


Wengine ni Saimon Msuva (Yanga), Erasto Nyoni (Azam fc), Himid Mao (Azam fc), Amri Kiemba (Simba), Haroun Chanongo (Simba), Salum Abubakary ‘Sure Boy’ (Azam fc), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Hamis Mcha ‘Vialli’ (Azam fc), Juma Luizio (Zesco United, Zambia), Mrisho Ngasa (Yanga), Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu (wote TP Mazembe, DR Congo).

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video