
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
MZAMBIA Patrick Phiri anatarajia kuiongoza Simba
sc katika mechi ya kwanza ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya
itakayopigwa leo jioni uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Kivutio kikubwa katika mechi ya leo ni
mshambuliaji wa Simba aliyesaini mkataba wa miezi sita kuitumikia klabu hiyo
akitokea kwa mahasimu wao Yanga sc, Mganda Emmanuel Anord Okwi.
Ingawa usajili wake una utata kwasababu uongozi wa
Yanga chini ya mwenyekiti wake, Yusuf Manji unadai una mkataba na Okwi, Simba
wanatarajia kumtumia nyota huyo wakiamini wako sahihi kumsainisha.
Kesi ya Okwi ipo Shirikisho la soka Tanzania TFF
na kinachosubiriwa ni tamko tu ili kujua Mganda huyo mwenye kasi uwanjani na
chenga za maudhi atakipiga wapi, Simba au Yanga.
Katika mazoezi ya Simba yaliyokuwa yakiendelea
uwanja wa Uninio, Bunju, jijini Dar es salaam, Okwi alikuwa kivutio kwa
mashabiki waliohudhuria kuona wachezaji wao.


Makamu wa Rais wa Simba sc, Geofrey Nyange 'Kaburu' (kushoto) akiwa na Okwi
Okwi alionekana kuwa na kasi uwanjani, alimiliki mpira, alikuwa anapiga chenga zake za maudhi na kusonga mbele.
Okwi alionekana kuwa na kasi uwanjani, alimiliki mpira, alikuwa anapiga chenga zake za maudhi na kusonga mbele.
Mara kadhaa mashabiki walikuwa wanampigia makofi
mazoezi kuashiria kukubali kwa kile anachofanya.
Baada ya mechi ya leo, kikosi cha Patrick Phiri
kitarejea Zanzibar kuendelea kumalizia program zake za maandalizi kabla ya ligi
kuanza septemba 20 mwaka huu.
Awali Simba walipanga kuchuana na Mtibwa Sugar,
lakini kocha Phiri akapendekeza kutafutiwa mechi ngumu ya kimataifa ili
kuangalia namna kikosi chake kilivyoimarika.
Viingilio katika mechi hiyo ni shilingi elfu 5
(5,000) kwa viti vya kijana, viti vya rangi ya chungwa ni shilingi 10,000, VIP
C na B itakuwa shilingi 2,000 wakati VIP A itakuwa shilingi elfu 30,000.
Tiketi kwa ajili ya mchezo huo zitaanza kuuzwa leo
kuanzia majira ya saa 4:00 asubuhi.
Simba wataanza kampeni za kusaka ubingwa wa ligi
kuu bara septemba 21 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam dhidi ya
Coastal Union.

0 comments:
Post a Comment