Saturday, August 16, 2014


Na Baraka Mpenja, Dar es salaam


MABINGWA wa zamani wa Tanzania kwa mwaka 1999 na 2000, Mtibwa Sugar wamekanusha taarifa zilizoenea mchana wa leo kuwa wameingia mkataba wa mwaka mmoja na aliyewahi kuwa kocha wa Simba sc, Mfaransa Patrick Liewig.

Leo mchana iliripotiwa kuwa Mtibwa imeamua kumchukua Liewig baada ya kuvutiwa na kazi yake akiwa Simba, lakini alifukuzwa mwaka juzi na mikoba yake kutua mikononi mwa mzalendo, Abdallah Kibadeni ‘King Mputa’.

Mkurugenzi wa Mtibwa Sugar, Jamal Bayser amesema taarifa hizo si za kweli, na wanachojua ni kwamba Mecky Mexime akisaidiwa na Zuberi Katwila na Patrick Mwangata ndio makocha wa klabu hiyo.

“Taarifa hizo ndio nazisikia, hakuna kitu kama hicho. Hutujawahi kuwa na mawasiliano na kocha huyo. Kocha wetu ni Mexime na anaendelea vizuri na maandalizi ya ligi kuu msimu ujao. Kikosi chetu kipo Dar es salaam kwasasa ”. Alisema Bayser.

Wakati huo huo, Mtibwa Sugar imetoka suluhu pacha ya bila kufungana na JKT Ruvu katika mechi ya kirafiki iliyopigwa jioni ya leo uwanja wa Bandari, Tandika, jijini Dar es salaam.


Mechi hiyo ilikuwa maalumu kwa makocha Mecky Mexime wa Mtibwa na Fredy Felix Minziro wa JKT Ruvu kupimana ubavu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video