Na Mwandishi Wetu
MAASKOFU
 wa makanisa mbalimbali nchini wametoa baraka zao za Tamasha la Krismas 
linalotarajia kufanyika Desemba 25 mwaka huu, kwenye uwanja wa Taifa 
jijini Dar es Salaam na baadaye kufanyika katika mikoa minne hapa 
nchini.
Viongozi
 hao wa makanisa nchini Tanzania kwa nyakati tofauti wameahidi kuliombea
 Tamasha la Krismas ili liwe la mafanikio yaliyotarajiwa kwa utukufu wa 
Mungu.
Wanasema 
 tamasha hilo ni muhimu hasa katika nyakati hizi za uasi mwingi ambapo 
dunia imekengeuka na kutenda matendo yanayomchukiza Mungu, kama vile 
vitendo vya ugaidi, uuzwaji wa madawa ya kulevya na mauaji ya watu wasio
 na hatia, hivyo tamasha hilo ili kurejesha utukufu wa Mungu mioyoni mwa
 watenda mabaya.
Tamasha
 la Krismasi ni muendelezo wa Tamasha la Pasaka lililoasisiwa tangu 
mwaka 2000 kwa lengo la kufikisha neno la Mungu kwa wananchi kwa njia 
muziki wa sifa na kuabudu. 
Hatua
 ya kuandaliwa kwa Tamasha la Krismasi ni baada ya kuwepo kwa matokeo 
mazuri ya kupungua kwa matukio mbalimbali ya uhalifu na ukiukwaji wa 
kanuni hapa nchini, hiyo ni kufuatia Tamasha la Pasaka ambalo mwaka huu 
lilikwenda na kauli mbiu ya utii wa sheria pasipo shuruti.
Utofauti
 wa Tamasha la Krismasi na Tamasha la Pasaka ni kwamba tamasha hili 
waimbaji wote wataimba moja kwa moja ‘live’ lakini maudhui yatabaki kuwa
 yale yale kama ya tamasha la Pasaka kumwabudu na kumtukuza Mungu kwa 
njia ya uimbaji.
Makamu
 Askofu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Dk. Magnus Mhiche
 anasema Mungu amempa mzigo mzito Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex 
Msama ambao anatakiwa awagawie waumini mbalimbali.
Sambamba na hilo Askofu Mhiche anampongeza Msama kwa hatua hiyo ya kuandaa matamasha ya kumtukuza na kumsifu Mungu.
Anasema
 tamasha hilo si la dhehebu moja bali  ni la Watanzania wote hivyo ni 
vema kujitokeza kwa wingi siku hiyo ili kuweza kuomba kwa pamoja kupitia
 nyimbo.
Pia
 Askofu Mkuu wa Kanisa la Oasis of Healing, Prosper Ntepa, pamoja na 
kuliombea tamasha hilo aliwapongeza waandaaji wa tamasha hilo, Kampuni 
ya Msama Promotions kwa kazi nzuri wanayoifanya katika uandaaji wa 
matamasha makubwa ya kumuabudu Mungu hapa nchini.
“Msama
 Promotions wanajitahidi katika uandaaji wa matamasha ya kumtukuza 
Mungu, tunazidi kumuombea afanikishe tamasha la krismas  ambalo 
linatarajia kufanyika kwenye mikoa mitano hapa nchini,” alisema Askofu 
Ntepa.
Askofu
 Ntepa pamoja na kutoa pongezi kwa Msama alitoa wito kwa waimbaji 
kutunga na kuimba nyimbo zenyemaudhui ya ujumbe mzito wenye tafsri 
halisi ya krismass,na mlengo wa kumtukuza na kumuabudu Mungu kwa njia ya
 sifa.
Askofu
 Ntepa anasema ili kufanikisha hilo waimbaji wanatakiwa kujitambua kwa 
jamii kwamba wanatakiwa kuwa mfano ambao utasaidia kufikisha neno la 
Mungu ambalo baadhi ya waimbaji  wanashindwa kwa sababu mbalimbali 
ikiwemo tamaa ya pesa.
Aidha
 Askofu Ntepa anasema ili Msama kufanikisha hilo inatakiwa kuchagua 
waimbaji ambao wana dhamira ya kweli ya kufikisha ujumbe wa neno la 
Mungu kwa waumini wengi zaidi.
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa
 la Living Water Centre, Onesmo Ndegi alitumia fursa hiyo kumpongeza 
Msama kwa kufanikisha tamasha hilo ambalo ni mfano wa kuigwa kwa sababu 
linafikisha ujumbe wa neno la Mungu kwa maelfu ya Watanzania.
Askofu
 Ndegi alisema yeye pamoja na viongozi wenzake wa dini pamoja na waumini
 wake wanaungana na kumuombea Msama kwa sababu ni wajibu  kama ilivyo 
agizwa kwenye Biblia,  kwani tamasha hilo ni ibada tosha kwa waliookoka 
 ingawa jamii inapata burudani na kumsifu Mungu kupitia nyimbo.
“Mimi
 na kanisa langu nawaunga mkono Msama Promotions zaidi na nazidi 
kuwaombea kufanikisha Tamasha la Krismasi kwa sababu wengi watashiriki 
 ibada ipasavyo,” alisema Askofu Ndegi.
Mwangalizi 
 Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima anasema jambo 
lolote la kumuimbia na kumuabudu Mungu kupitia nyimbo ni jema.
Gwajima
 anawashambulia wale wote watakaotumia tamasha hilo kama sehemu uiba 
fedha kwani anaamini fedha zitakazopatikana kwenye tamasha hilo 
litasaidia jamii mbalimbali ya Watanzania kama ilivyoagizwa na mwandaaji
 ambaye ni Msama.
 “Tamasha
 la Krismasi ni sehemu ya mahubiri kwani kila anayehubiri anatakiwa 
kuyatekeleza yale anayoyahubiri  na si vinginevyo,” anasema Gwajima na 
kuongeza;
“Namuombea Msama na kampuni zake kufanikisha matamasha yake ambayo ni sehemu stahili katika kumtukuza na kumuabudu Mungu,”.
Mchungaji
 Christopher Mlaponi wa (TAG) Kinondoni Revival aliipongeza Msama 
Promotions kwa sababu wao ndiyo waandaaji wakuu wa Matamasha ya 
Kimataifa ya muziki wa injili kwa hatua waliyofikia.
Mchungaji
 Christopher, anasema kampuni hiyo inastahili pongezi kwa kuanzisha 
Tamasha la Krismasi kwa kuwa lina manufaa makubwa katika jamii hasa 
katika siku hizo za sikukuu ya Krismasi.
Anasema
 jambo la busara kwa kampuni hii kuanzisha matamasha ya muziki wa injili
 kwa siku kama hizi ambapo aliwataka waumini kuitumia siku hiyo 
kusheherekea Krismasi kwa kumtukuza Mungu kwa kushiriki katika tamasha 
hilo na si kufanya vitendo viovu.
“Hii
 siku siyo ya kula na kunywa, au kufanya anasa hapana, isipokuwa watu 
wanatakiwa kwenda makanisani asubuhi kama inavyohitajika wakirudi 
wajumuike katika Tamasha la Krismasi kwani wanapata neno la Mungu 
kupitia nyimbo za injili” anasema .
Anasema hiyo siku hutokea mara moja kwa mwaka hivyo Wakristo wanatakiwa wamtukuze na kumuimbia Yesu kwenye tamasha hilo.
Naye
 Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama anasema tamasha hilo ni 
muendelezo wa Tamasha la Pasaka, hivyo wadau wajiandae kupata ibada 
stahiki kwa waumini mbalimbali watakaofika uwanja wa Taifa jijini Dar es
 Salaam  na wengine wa mikoa minne hapa nchini ambayo ni Morogoro, 
Dodoma, Tanga na Arusha.
“Tamasha
 la mwaka huu litashirikisha waimbaji mbalimbali wa Tanzania na nje, 
lengo likiwa ni ibada ambayo itawafikia waumini wote,” anasema Msama.
Msama
 anawataja waimbaji waliothibitisha kushiriki katika tamasha hilo ni 
pamoja na Rose Muhando, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro na Eiphreim 
Sekereti huku waimbaji wengine wanaendelea na mazungumzo kwa ajili ya 
kuthibitisha kushiriki.





0 comments:
Post a Comment