Kocha
 mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage akitoa somo kwa makocha 
wanashiriki kozi ya ukocha ngazi ya pili ndani ya darasa kwenye Ukumbi 
wa Harbours Club, Kurasini.  
 
 
 
Kocha mkuu wa Twiga Stars akitoa somo kwa makocha wa kozi ya ngazi ya pili kwa vitendo
KOZI
 ya makocha wa ngazi ya pili (Intermediate) inayosimamiwa na Chama cha 
Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), inatarajiwa kufungwa 
Jumanne ijayo baada ya kudumu kwa wiki nne. 
Kozi
 hiyo ilianza Juni 3 mwaka huu kwenye Ukumbi wa Harbours Club, uliopo 
Kurasini chini ya Mkufunzi Rogasin Kaijage, ambaye ni Kocha wa timu ya 
Taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’ ambapo makocha mbalimbali pamoja na 
wachezaji wa zamani wamejitokeza kushiriki. 
Ofisa
 Habari wa DRFA, Mohamed Mharizo alisema kozi hiyo imekuwa na mafanikio 
na wanatarajia makocha walioshiriki katika kozi hiyo watakuwa na mchango
 mkubwa katika kuendeleza mpira wa miguu katika mkoa wa Dar es Salaan na
 Taifa kwa ujumla.
“Hadi
 sasa tunashukuru kuona tunafanikisha kozi hii ambayo wengi wameitikia 
wito, mwisho wa kozi hii ndio mwanzo wa kozi nyingine.
“Lakini
 haya ya kozi ya makocha ni moja ya majukumu ya Kamati ya Ufundi ya DRFA
 yaliyoainishwa katika Katiba, hivyo hili ni moja ya shabaha yetu na 
mengine mengi mazuri yanafuata,” alisema Mharizo.
 Kozi
 hiyo ni ya kwanza kuendeshwa na DRFA tangu kuingia madarakani kwa 
uongozi mpya wa chama hicho Desemba 12, chini ya Mwenyekiti wake Almas 
Kassongo.






0 comments:
Post a Comment