Saturday, August 16, 2014

Pure joy: The Tottenham players run over to celebrate with their jubilant fans after Dier's late winner
LIGI kuu soka nchini England imeanza leo  kwa mechi saba kupigwa katika viwanja tofauti.

Mechi ya mapema ilishuhudiwa katika dimba la Old Trafford ambapo wenyeji Manchester United chini ya kocha mpya, Mholanzi, Louis Van Gaal walilala 2-1 dhidi ya Swansea City.

Katika mechi nyingine za Jioni, Leicester City wakiwa nyumbani wamelazimisha sare ya mabao 2-2 dhidi ya Everton.

QPR wakiwa nyumbani wamechapwa bao 1-0 na Hull City, wakati Stoke City nao wamelala 1-0 wakiwa uwanja wa nyumbani dhidi ya Aston Villa.

Katika mechi nyingine West Brom wametoka sare ya mabao 2-2 na Sunderland.

Tottenham wakiwa ugenini wameshinda bao 1-0 dhidi ya wenyeji West Ham United.

Mechi ya mwisho leo hii inaendelea baina ya Asernal dhidi ya Crystal Palace katika uwanja wa Emirates mjini London.

Ligi hiyo itaendelea kesho ambapo washindi wa pili wa msimu uliopita, Liverpool watakuwa katika dimba lao la Anfield kuchuana na Sounthampton, wakati mabingwa Manchester City wataoneshana kazi ugenini na Newcastle United.


Jumatatu ya wiki ijayo, Jose Mourinho ataiongoza Chelsea kuanza na timu mpya ya Burnley.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video