Saturday, August 16, 2014

Na Baraka Mpenja

MABINGWA wa Tanzania bara, Azam fc watachuana na El Merreikh ya Sudan katika mchezo wa robo fainali ya klabu bingwa Afrika mashariki na kati, kombe la Kagame siku ya jumatano kwenye uwanja wa Nyamirambo, mjini Kigali, nchini Rwanda.

Hii inatokana na wenyeji Rayon Sports kumaliza kundi A wakishika nafasi ya kwanza kwa kujikusanyia pointi 10 kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Altabara ya Sudan kusini.

Bao pekee la ushindi la Rayon limefungwa katika dakika ya 87 kupitia kwa Motombo Govin.

Kwa matokeo ya leo, kundi A linaongozwa na Rayon wenye pointi 10, wakifuatiwa na Azam fc waliojikusanyia pointi 8 katika nafasi ya pili, huku Altabara wakishika nafasi ya tatu kwa pointi 3 na wanakwenda Robo fainali pia.

Rayon inaweza kukabiliana na KCC ya Uganda au APR ya Rwanda kutegemeana na matokeo ya mechi za mwisho katika kundi B hapo kesho.

Mapema katika uwanja huo wa Nyamirambo, Azam fc walijizolea pointi tatu muhimu dhidi ya Adamma City ya Ethiopia baada ya kuitungua mabao 4-1.

Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilimalizika kwa sare ya bao 1-1 ambapo Azam walikuwa wa kwanza kufunga kupitia kwa Bocco akiunganisha krosi ya Khamis Mcha ‘Vialli’, lakini  Desaleny Bebesh aliisawazishia Adamma katika dakika ya 39.

Katika dakika 55, Kavumbagu alifunga bao la pili akimalizia krosi ya Erasto Nyoni.


Dakika ya 60 Mcha alifunga bao la tatu baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na mlinda mlango wa Adamma na katika dakika ya 74 Tchetche alihitimisha karamu ya mabao.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video