
Na Baraka Mpenja, Dar es
salaam
Imechapishwa Julai 5, 2014, saa 4:42 asubuhi
BAADA ya mapumziko ya kutoona mechi za ligi kuu katika dimba la
Kumbukumbu ya Sokoine, jijini Mbeya, wapenzi wa soka leo hii watajikumbushia
ladha ya soka kwa kuzishuhudia Mbeya City fc na Tanzania Prisons zikichuana
vikali.
Hii ni mechi maalum ya kajaribu mfumo wa tiketi za elekroniki
katika dimba hilo na inatarajia kuanza majira ya saa 10 kamili jioni.
Mbali na kuwa mechi ya kirafiki, pia itatoa fursa kwa wapenzi wa
timu hizi kuona vikosi vyao wakati huu maandalizi ya ligi kuu soka Tanzania
bara yakiendelea kushika kasi.
Shirikisho la soka Tanzania, TFF, lilitangaza kiingilio cha mechi
hiyo kuwa ni shilingi elfu tatu kwa majukwaa yote ambapo tiketi zilianza kuuzwa
julai mosi mwaka huu kupitia M-Pesa, CRDB Simbanking na maduka ya Fahari
Huduma.
Wakati huo huo, jana, julai 4 mwaka huu, shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF) liliendesha mafunzo ya matumizi ya tiketi za elektroniki
kwa wadau wa mpira wa miguu mkoani Mbeya.
Mafunzo hayo yalifanyika kwenye Uwanja wa Sokoine, na kushirikisha
wasimamizi wa mechi, viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA)
na makatibu na maofisa habari wa klabu za Tanzania Prisons na Mbeya City.
Wengine walioshiriki mafunzo hayo ni Meneja wa Uwanja wa Sokoine
na msaidizi wake, wasimamizi wa milangoni (stewards) na waandishi wa habari wa
mkoani Mbeya.

0 comments:
Post a Comment