Saturday, July 5, 2014

Mshambuliaji Brain Umony (kushoto) ameachwa na Azam fc

Na Baraka Mpenja Dar es salaam


Imechapishwa Julai 5, 2014, saa 3:30 asubuhi

MABINGWA wa soka Tanzania bara, wana Lambalamba Azam fc wamevunja mkataba na mshambuliaji wao raia wa Uganda, Brian Umony.

Umony hayupo kwenye mipango ya kocha mkuu wa klabu hiyo, Mcameroon, Joseph Marius Omog, hivyo uongozi umelazimika kuachana naye.

Afisa habari wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga amesema Umony baada ya kuitumikia Azam kwa mwaka mmoja na nusu ama miwili, wameamua kuachana naye kwa amani na kumpati stahiki zake.

“Uongozi wa Azam umekaa na mchezaji huyo na kuvunja mkataba wake. Kwa maana hiyo amepata stahiki zake na amekwenda mbele katika maisha yake ya mpira”.  Alisema Jafar.

“Ni kawaida  kwenye  mpira kuwa, yule anayesitishiwa mkataba wake anatakiwa apewe haki yake. Wengine wanamuacha halafu hawampi haki yake na ndio maana unaona mchezaji anakwenda kushitaki TFF au FIFA. Sisi tunamwambia mchezaji, tunakaa naye na tunakubaliana na kumpa haki yake”.

Hata hivyo, Jafar alisema wana nafasi moja ya kusajili mchezaji mmoja wa kimataifa na kama watapata kifaa kipya basi watafanya hivyo, japokuwa sio lazima kumaliza nafasi zote.


Afisa habari huyo alisema kikosi chao kinaendelea vizuri na maandalizi ya ligi kuu soka Tanzania bara inayotarajia kuanza kushika kasi mwezi agosti mwaka huu pamoja na ligi ya mabingwa barani Afrika.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video