Monday, May 26, 2014



http://images.supersport.com/2014/5/RuudKrol-LOOKS131113BBP300.jpg
NAHODHA wa zamani wa Uholanzi katika fainali za kombe la dunia, Ruud Krol amefukuzwa kazi ya ukocha mkuu katika klabu ya Tunisia ya Esperance ikiwa ni wiki kadhaa zimepita tangu awaongoze kutwaa ubingwa wa ligi kuu katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
Krol amefukuzwa kazi saa kadhaa baada ya timu yake kufungwa mara ya pili mfululizo katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika mwishoni mwa wiki, na taarifa ya klabu imesema Mfaransa Sebastien Desabre atatangazwa kuwa mrithi wake.
Kocha huyo mwenye miaka 65 amekuwa kocha wa kwanza nchini Tunisia kushinda mataji ya mawili  akiwa na klabu mbili tofauti baada ya kuwapa ubingwa Esperance dhidi ya timu yake ya zamani ya SC Sfaxien mapema mwezi huu.
Krol aliachana na SC Sfaxien mwezi novemba mwaka jana baada ya kuwaongoza kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Tunisia na kombe la shirikisho.
Mwezi Oktoba na Novemba mwaka jana, Mholanzi huyo pia aliiongoza kwa muda timu ya taifa ya Tunisia dhidi ya Cameroon katika mchezo wa kufuzu fainali za kombe la dunia. Cameroon ilishinda kwa wastani wa mabao 4-1.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video