LIGI kuu nchini Uturuki haina jina kubwa ukilinganisha
na ligi zenye mvuto mkubwa barani ulaya kama vile England, Hispania, Ujerumani
na Italia.
Kutokana na hali hiyo, kiungo mshambuliaji wa
mabingwa wa Uturuki, klabu ya Galatasaray, Mholanzi Wesley Sneijder ameanza
kuonekana wa kawaida sana na kuwa hatarini kulikosa kombe la dunia mwaka huu
nchini Brazil.
Sneijder alikuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha
Uholanzi, lakini mambo yamebadilika baada ya kwenda Uturuki na sasa kocha mkuu wa
timu ya Taifa ya Uholanzi, Louis Van Gaal amekaririwa akisema kuwa nyota huyo
yawezekana asijumuishwe katika kikosi chake.
Baada ya maneno ya kocha Gaal, wachezaji wenzake
wanasemaje juu ya maamuzi ya kumuacha Sneijder?
Winga machachari wa klabu ya Bayern Munich na timu
ya Taifa ya Uholanzi, Arjen Robben amemkazia bosi wake na kusema
Sneijder bado ni mtu muhimu katika kikosi chao na anaweza kuisaidia nchini yake.
Sneijder bado ni mtu muhimu katika kikosi chao na anaweza kuisaidia nchini yake.
“Wesley ni mchezaji muhimu. Nilishaongea hili toka mwanzo na sio
siri kuwa namkubali sana jamaa”.
“Anapocheza katika kiwango chake ambacho anacheza sasa, Wesley
ni mchezaji anayeongeza kitu cha ziada katika timu. Unahitaji mchezaji kama
yeye kombe la dunia”.
“Nampenda sana Wesley. Kiukweli hatuwezi kufananisha kiwango
chake cha miaka minne iliyopita. Umri unakwenda na mambo yanabadilika. Lakini
bado anaongeza kitu Fulani kwa timu yetu”. Amesema Robben.
Sneijder ameichezea mechi 97 timu ya Taifa ya Uholanzi na
kufunga mabao 26.


0 comments:
Post a Comment