Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail.com
Wakati
 mashabiki wengi wakidhani Mabingwa wa soka duniani, timu ya taifa ya 
Kispania wangewafunga Tahiti mabao zaidi ya 10, hatimaye watoto wa 
Tahiti wamekaza na kuwazuia vilivyo wapinzania wao na kufungwa maboa 
10-0 tu.
Mshambuliaji 
 Fernando Torres amefunga mabao manne pamoja na kukosa penalti wakati 
Hispania ikiifumua 10-0 Tahiti katika mchezo wa Kundi B Kombe la Mabara.
Alifunga
 mabao hayo katika dakika za tano, 33, 57 na 78 wakati David Villa 
alipiga Hat-trick katika dakika za 39,49 na 64, David Silva akafunga 
mawili dakika za 31 na 89 na Juan Mata pia akafunga dakika ya 66 
kuiwezesha Hispania kupaa kileleni mwa Kundi B mbele ya Nigeria, ambao 
muda huu wanamenyana na Uruguay.
Kikosi
 cha Hispania kilikuwa: Reina, Albiol, Azpilicueta, Ramos/Navas dk46, 
Monreal, Martinez, Cazorla/Iniesta dk76, Silva, Villa, Torres na 
Mata/Fabregas dk69.
Tahiti:
 Roche, Ludivion, Vallar, Lemaire/Vero dk73, Aitamai, J Tehau, A Tehau/T
 Tehau dk53, Vahirua, Caroine, Bourebare/L Tehau dk69 na Chong Hue.
 
 
Moto wa nguvu: Fernando Torres alikuwa hatari katika mchezo wa usiku wa kuamkia leo dhidi ya Tahiti
 
 
Hata mie: Mshambuliaji Barcelona  David Villa  naye alionesha kiwango cha juu
 
 
Kazi yaanza: Torres akitumbukiza goli la kwanza 
CONFEDERATIONS CUP GROUP B
| Team | Played | Won | Drawn | Lost | For | Against | Points | 
|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Spain | 2 | 2 | 0 | 0 | 12 | 1 | 6 | 
| Nigeria | 2 | 1 | 0 | 1 | 7 | 3 | 3 | 
| Uruguay | 2 | 1 | 0 | 1 | 3 | 3 | 3 | 
| Tahiti | 2 | 0 | 0 | 2 | 1 | 16 | 0 | 
 
 
Lingine tena: Torres akiandika kimiani bao la pili





0 comments:
Post a Comment