Omary
 Tego yumo ndani ya kundi jipya la Raha ya Pwani Modern Taarabu chini ya
 usimamizi wa mkurugenzi wa kampuni ya KFM, inayomiliki kituo cha redio 
cha kifimbo fm kinachana anga kutoka kanda ya kati, Dodoma Tanzania, 
Dkt. Kifimbo
Na Baraka Mpenja 
Haya
 haya wakazi wa Dodoma, baada ya kusikia burudani nyingi za miondoko ya 
kipwani Pwani kutoka makundi mbalimbali, sasa wapenzi wa taarabu 
wanajiandaa kupata burudani ya kukata na shoka kutoka kundi jipya la 
“Raha ya Pwani Modern Taarabu” chini ya usimamizi wa kampuni ya KFM 
inayojihusisha na masuala ya mawasiliano kwa umma.
Mkurugenzi
 wa kampuni ya KFM  inayomiliki kituo cha redio cha Kifimbo Fm 
kinachorusha matangazo yake kutoka mjini Dodoma maarufu kama Kanda ya 
kati,  Dkt. Kifimbo ameimbia MATUKIO DUNIANI kuwa licha ya kampuni 
yake kujihusisha na masuala ya mawasiliano kwa umma, imeamua kujikita 
katika masuala ya burudani ili kuwapa mashabiki wake kitu roho inapenda 
katika ulimwengu wa muziki wa taarabu.
“Unajua
 watanzania wengi wanapenda masuala ya burudani, Kwa kutambua hilo, 
kampuni yetu imeamua kuanzisha kundi jipya la muziki wa taarabu 
lijulikanalo kwa jina la `Raha ya Pwani Modern Taarabu` ili kukonga 
nyoyo za mashabiki wa redio yetu na watanzania wote kwa ujumla”. Alisema
 Dkt. Kifimbo.
Dkt.
 Kifimbo amesema uzinduzi rasmi wa kundi hili lililosheheni vipaji vya 
kutosha utafanyika Julai 28 (mwezi wa saba) mwaka huu, katika ukumbi wa 
burudani wa Kilimani Dodoma.
“Watu
 wakae mkao wa kula, kundi hili litatoa burudani ya kutosha kwa 
mashabiki wa taarabu. Kuna waimbaji wenye vipaji vikubwa wakiwemo 
wakongwe na vijana. Yumo Mwanahawa, Shakira, Omary Tego, Issa Kamongo, 
Abubakar Mzuri na Hassan Ally. Kuwepo kwa waimbaji hawa, Raha ya Pwani 
Modern Taarabu lazima itese mjini”. Alisisitiza Dkt. Kifimbo.
Mkurugenzi
 huyo wa KFM aliwataka mashabiki wa muziki wa taarabu kujitokeza kwa 
wingi siku ya uzinduzi, kwani “Mwenye macho haambiwi tazama”, wasingoje 
kusimuliwa.



0 comments:
Post a Comment