Waziri
 wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki akifungua mkutano wa 
Shirika la Hifadhi za Mbuga za Taifa TANAPA na wahariri wa vyombo vya 
habari kuhusu Wajibu wa vyombo vya habari katika kukabiliana na Ujangili
 katika hifadhi za taifa unaofanyika kwenye ukumbi wa Siasa na Kilimo 
Ofisi za Manispaa ya Iringa, Balozi Kagasheki amewaasa wahariri wa 
vyombo vya habari kujadiliana kwa undani suala zima la kukomesha 
ujangili na jukumu la wanahabari katika mkakati huo wakishirikiana na 
serikali kwa ujumla kupitia taasisi za ulinzi katika mbuga za wanyama, 
amewataka wahariri kuwa wabunifu kwa kuandika makala na habari za 
kiuchunguzi ili kuibua mbinu hizo chafu na majangili ili kutokomeza 
ujangili huo na kupata ufumbuzi kamili wa changamoto hizo za ujangili, 
ameongeza kwamba wizara yake iko tayari kupokea maoni mbalimbali kutoka 
kwa wahariri na wadau mbalimbali yatakayofanikisha kupata ufumbuzi wa 
kutokomeza kabisa ujangili katika mbuga na pia amejiwekea utaratibu wa 
kukutana na waandishi wa habari kila mwezi atakutana na vyombo vya 
habari ili kuzungumza na wanahabari kuhusu masuala mbalimbali ya wizara 
hiyo.PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE- IRINGA 
 
 
Wahariri mbalimbali wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki wakati akifungua mkutano huo. 
 
 
Wahariri
 wa vyombo mbalimbali vya habari wakiwa makini katika kusikiliza wakati 
Waziri Balozi Khamis Kagasheki akizungumza katika mkutano huo. 
 
 
Balozi Khamis Kagasheki akisisitiza jambo wakati akifungua mkutano huo kwenye ukumbi wa Siasa na Kilimo mjini Iringa 
 
 
Mkuu
 wa mkoa wa Iringa Dr. Christine Ishengoma akizungumza katika mkutano 
huo wakati akimkaribisha Waziri wa Malisiali na Utalii Mh. Balozi Khamis
 Kagasheki.
Waziri wa Malisili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki akiongozana na 
Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr. Christine Ishengoma wakati akiwasili katika 
ukumbi wa mikutano wa Siasa na Kilimo mkoani Iringa ambako mkutano wa 
Wahariri wa vyombo vya habari na Shirika la Hifadhi za mbuga za Taifa 
TANAPA unafanyika. 
Mwenyekiti
 wa Kamati ya kudumu ya bunge ya Ardhi Mazingira Ndugu James Lembeli 
akiingia kwenye ukumbi wa mkutano huku akiwa ameongozana na Mkurugenzi 
wa TANAPA Ndugu Allan Kijazi kushoto. 
 
Mwenyekiti
 wa Kamati ya kudumu ya bunge ya Ardhi Mazingira Ndugu James Lembeli 
akiingia kwenye ukumbi wa mkutano huku akiwa ameongozana na Mkurugenzi 
wa TANAPA Ndugu Allan Kijazi kushoto. 
 
Waziri
 wa Maliasili na utalii Balozi Khamis Kagasheki wa pili kutoka kulia 
akiwa katika mkutano huo kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi
 na Mazingira Ndugu James Lembeli na kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa 
TANAPA Ndugu Allan Kijazi na Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr. Christine 
Ishengoma. 
 
 
Waziri
 wa Maliasili na utalii Balozi Khamis Kagasheki katikati akiwa katika 
mkutano huo kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya bunge ya Ardhi na Mazingira
 Ndugu James Lembeli na kushoto ni mkuu wa mkoa wa Iringa Dr. Christine 
Ishengoma 
 
 
Waziri
 Kivuli wa Wizara ya Maliasili na Utalii Mbunge wa Iringa mjini 
Mchungaji Peter Msigwa akizungumza katika mkutano huo huku Waziri wa 
Maliasili Balozi Khamis Kagasheki wa pili kutoka kushoto akisikiliza, 
wengine ni Ndugu James Lembeli Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi na
 Mazingira na kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr. Christine Ishengoma. 
Mwenyekiti
 wa Kamati ya bunge ya Ardhi na Mazingira Ndugu James Lembeli 
akizungumza katika mkutano huo huku waziri wa Maliasili na Utalii Balozi
 Khamis Kagasheki akisikiliza kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr. 
Christine Ishengoma. 
Mkurugenzi
 wa TANAPA Ndugu Allan Kijazi akizungumza katika mkutano huo kukaribisha
 wageni mbalimbali waliohudhuria mkutano huo unafofanyika kwenye ukumbi 
wa Siasa na Kilimo mjini Iringa
Mwenyekiti
 wa Kamati ya bunge ya Ardhi na Mazingira Ndugu James Lembeli 
akizungumza katika mkutano huo huku waziri wa Maliasili na Utalii Balozi
 Khamis Kagasheki akisikiliza kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr. 
Christine Ishengoma. 
Mkurugenzi
 wa TANAPA Ndugu Allan Kijazi akizungumza katika mkutano huo kukaribisha
 wageni mbalimbali waliohudhuria mkutano huo unafofanyika kwenye ukumbi 
wa Siasa na Kilimo mjini Iringa
 

0 comments:
Post a Comment