Tuesday, April 16, 2013

mgambo vs yanga
Kiungo nyota Haruna Hakizimana Fadhili Niyonzima `Fabrigas` akiwahadaa mabeki wa Mgambo kwenye moja ya mechi walizokutana siku za nyuma

Na Baraka Mpenja
Vinara wa ligi kuu Tanzania bara, vijana wa mitaa ya Jangwani na Twiga Dar Young Africans tayari wapo jijini Tanga “waja leo waondoka leo” kujiandaa na mchezo wa kesho wa ligi kuu soka Tanzania bara katika dimba la CCM Mkwakwani dhidi ya wapiga kwata wa Mgambo JKT.

AKizungumza kutoka Tanga Afisa habari wa klabu hiyo Baraka Kizuguto,  amesema kikosi cha Yanga kiliwasili jana mkoani humo tayari kwa kuziwinda pointi tatu muhimu mbele ya maafande hao wa jeshi wanaopigania uhai wa kubakia ligi kuu msimu huu.

“Wachezaji wote wapo salama kabisa, hatuna majeruhi hata mmoja hivyo ni wakati mwingine muhimu kwetu kutafuta ushindi wa ugenini na kuzidi kuwatimulia vumbi wanaotufuata nyuma yetu katika harakati za kuwania taji la ligi kuu msimu huu”. Alisema Kizuguto.

Kizuto aliongeza kuwa mchezo huo ni mgumu sana kutokana na mazingira halisi ya Mgambo ambao wanapigana kufa na kupona wakihitaji mzigo wa pointi tatu ili kujiweka mazingira mazuri katika msimamo wa ligi kuu msimu huu ambao Yanga wanatesa kileleni.

“Ushindi na lazima, mashabiki wetu wasiwe na hofu na wajitokeze kwa wingi kushuhudia kikosi bora cha Yanga kilichoweka kambi nchini Uturuki na sasa kuvuna matunda yake mzunguko huu wa pili wa ligi kuu”. Aligamba Kizuguto.

Yanga wamebakiza mechi nne tu na kati ya hizo wanahitaji ushindi wa mechi mbili kuanzia ya kesho ili kujitangazia ubingwa.

Mechi walizobakiza ni ya Coastal unioni uwanja wa Mkwakwani, Ruvu JKT uwanja wa Taifa, Wekundu wa msimbazi Simba uwanja wa Taifa pamoja na mechi ya kesho dhidi ya Mgambo.

Kati ya mechi hizo zilizobaki wanajangwani hao wana kibarua kizito mbele ya Simba na Coastal kutokana na ubora wa timu hizo, lakini kwa upande wa JKT Ruvu na Mgambo kuna uwezekano wa Yanga kunyakua pointi kufuatia timu hizo kufanya vibaya katika mechi zake nyingi.

Wakati Yanga wakijinasibu kuvuna mzigo wote wa pointi tatu, nao Mgambo JKT kupitia kwa katibu mkuu wake Antony Mgaya wamesema kuwa watapambana kufa na kupona katika mchezo wa kesho ili kupata ushindi baada ya kupoteza mchezo uliopita kwa kufungwa 1-0  na Prisons jijini Mbeya.

Mgaya alisema wanajua Yanga msimu huu wana timu nzuri lakini hii haiwaogopeshi kupambana kwani kwenye soka lolote huwa linaweza kutokomea.

“Mgambo na Yanga kwa majina hakuna ushindani, lakini soka lina maajabu yake, tunaweza kushinda na kuwashangaza wengi, Kocha Kampira amewaandaa vijana kwa ajili ya ushindani”. Alisema Mgaya.

Mgambo JKT wapo nafasi ya 10 wakijikusanyia pointi 24 na juu yao wapo wanajelajela Tanzania Prisons wenye pointi 26 ambao kwa upande wao wanaonekana kujinusuru kushuka daraja msimu huu baada ya mapambano ya muda mrefu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video