Friday, April 12, 2013



Na Baraka Mpenja
Mkakati wa kuwarudisha upya katika soka la ushidani mabingwa wa zamani wa Tanzania mwaka 1986, Tukuyu stars “Banyambala” unazidi kushika kasi huku mpango wa muda mfupi wa kuisajili timu hiyo kucheza ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa ukiwa umekamilika.
Akizungumza na mtandao huu kwa njia ya simu kutoka wilayani Rungwe mkoani Mbeya, katibu mkuu wa chama cha soka wilayani humo, Enzi Wiliam Seme, amesema sasa Banyambala wapo ligi daraja la tatu jijini Mbeya .
Seme amesema katika michuano ya ligi hiyo, wamefuzu hatua ya sita bora na sasa wakishika nafasi ya pili wakiwa na Pointi 5 nyuma ya vinara wa ligi hiyo klabu ya Magereza Ruanda waliojikusanyia pointi 6 kibindoni.
Katibu huyo alisema hapo jana walionesha umwamba wao kwa kuwatungua Kimondo mbozi mabao 2-1 na kuzidi kujiweka sawa kuingia ligi daraja la pili ngazi ya taifa.
“Unajua wakati tunazindua mkakati wa kuifufua klabu yetu, tuliweka mipango ya muda mfupi na mrefu, mpango wa kwanza ulikuwa kuisajili timu icheze ligi daraja la tatu, sasa tumekamilisha, tunachohangaika sasa ni kusonga mbele zaidi katika ligi hiyo”. Alisema Seme.
Seme aliongeza kuwa hatua ambayo inaendelea kwa sasa ni kubadilisha katiba ya klabu hiyo kutoka mfumo wa ridhaa kwenda kampuni ili kukaribisha wadau wenye nia ya kununua hisa kufanya hivyo mara moja.
“Tunataka timu yetu iwe bora na kitalu cha kuzalisha wachezaji, hatua muhimu pia ni kuiongoza kisasa, ndio maana tunafanya mchakato wa kuibadili katiba yetu ili kuwapa nafasi wenye fedha zao kununua hisa na kuimarisha klabu yetu”. Aliongeza Seme.
Pia katibu huyo alisifu serikali ya wilaya chini ya  mkuu wa wilaya Chrispin Meela, kuwa inahaha huku na huku kuhakikisha inapata wadhamini wa kuiwezesha timu hiyo kurejea rasmi katika soka la Tanzania na kimataifa.
Seme alijigamba kuwa chini ya Meela hakuna kinachoharibika, lazima watanzania wawaone kwa mara nyingine Tukuyu stars wakitanda anga za soka la Tanzania.
Pia kiongozi huyo aliongeza kuwa wanajipanga kufanya mkutano wa pamoja na wachezaji wa zamani wa klabu hiyo wakiwemo Godwirn Aswile, Moses Mkandawile, Willy Martin na wengineo ili kuona wamefikia wapi na mkakati wao wa kuisaidia klabu hiyo kurejea tena.
Tukuyu stars ni moja kati ya klabu zilizokuwa na jina kubwa sana nchini Tanzania kutokana na umoja wa wakazi wa Mbeya, wachezaji wake maarufu kama ‘Banyambala` pamoja na na viongozi wa serikali ambao walihamasisha kuishangilia timu hiyo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video