Friday, April 12, 2013



Na Baraka Mpenja
Uongozi mpya wa Chama cha kandanda mkoani Ruvuma (FARU) umejipanga kuwekeza katika soka la vijana ili kuunga mkono mpango wa shirikisho la soka  Tanzania TFF ulizinduliwa hivi karibu na Rais wake Leodigar Chila Tenga kwa lengo la kuwekeza katika soka hilo kwa mwaka 2013-2016.
Mwenyekiti wa chama hicho Golden Singaone, amesema viongozi wengi wa chama hicho ukimwondoa katibu mkuuu wake ni wapya kabisa, hivyo wamekuja na mipango mingi ya kuboresha Mpira wa miguu mkoani humo hususani soka la vijana.
Singaone alisema uongozi huo umeyakuta mashindano pekee ya Coca Cola, lakini sasa wanafanya mipango ya kutafuta udhamini ili kuwa na mashindano mengi zaidi kama sehemu ya  kuwaweka pamoja vijana kwa muda mrefu.
“Mimi binafsi licha ya kuwa mwenyekiti wa chama, pia ni mdau mkubwa wa soka la vijana na ndio maana kila mwaka ninaendesha mashindano ya viaja ya `Singaone Cup, kwakweli tunajipanga kufanya mambo ya maana sana”.  Alisema Singaone.
Kiongozi huyo aliongeza kuwa TFF imeonesha njia nzuri ya kuthamini soka la vijana ambalo kwa sasa ndio msingi wa timu ya taifa iliyojaza makinda wengi, endapo juhudi hizi zitaendelezwa, taifa litanufaika sana na aina ya wachezaji watakaopatikana.
“Kikubwa ni kutafuta fedha za kutosha ili mambo yaende sawa, soka linahitaji uwekezaji na kama tutapata watu wa kutambua umuhimu wa jambo hili, basi itasaidia sana kujenga misingi bora ya soka letu”. Aliongeza Singaone.
Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa licha ya kuanza mikakati hiyo, pia wana mikakati mizito ya kuisaidia klabu maarufu mkoani humo na Tanzania nzima, Maji maji Fc  “wanalizombe” ili wasajili wachezaji makini na kupata makocha wa kiwango cha juu.
Kwa upande wake meneja wa Majimaji FC Godfrey Ambrose Mvula maarufu kama “Makete” amesema wameandaa tukio maalumu aprili 27 mwaka lililopewa jina la “Maji maji day”  kwa lengo la kuwakutanisha wadau wa soka mkoani Ruvuma ili kuhamasishana  kuichangia timu hiyo kwa ajili ya ligi daraja la kwanza msimu ujao.
“Siku hiyo ni muhimu sana kwetu wana Ruvuma, tunafikiri kuwaalika baadhi ya wachezaji wa zamani na wasanii maarufu wa mkoa wetu, Abdallah Kibaden, Madaraka Seleman `mzee wa kiminyio`, wasanii kama Joseph Haule `Profesa Jay` na wengine wengi  wanatarajiwa kualikwa siku hiyo ili kupamba tamasha hilo kubwa”. Alisema  Mvula.
Mvula alisema baada ya tukio hilo, wanajipanga kufanya usajili wa wachezaji wapya ambao watachanganya damu, yaani chipkizi na wazoefu ili waimarishe klabu hiyo.
Meneja huyo aliongeza kuwa wachezaji wengi watawatoa katika mashindano ya Coca Cola mwaka huu huku wakifanya juhudi ya kupata makocha wa kiwango cha juu ili waiunganishe timu hiyo.
Mvula alisisitiza kuwa kinachowasumbua sana wana Lizombe ni ukata, sasa wanajitahidi kupanga mipango ya kupata fedha wakisaidiwa na mkuu wa mkoa huo, Said Mwambungu anayewatafutia wadhamini.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video