Friday, April 12, 2013



Na Baraka Mpenja
Mabingwa wa kombe la Kagame na Vinara wa ligi kuu soka Tanzania bara, klabu ya Yanga ya Dar es salaam yenye makazi yake mitaa ya Twiga na Jangwani  kesho inatarajia kushusha daluga zake za wanaume kumi na mmoja  dhidi ya maafande wa jeshi la kujenga taifa kutoka jijini Arusha “Geneva ya Afrika”, klabu ya JKT Oljoro, mchezo utakaopigwa uwanja wa taifa majira ya saa kumi kamili jioni.
Akizungumza na matandao huu, Afisa habari wa klabu hiyo “Kwalalumpa Malysia”, Baraka Kizuguto  amesema mchezo huo ni muhimu sana kwao ingawa mabadiliko ya ratiba yamewaathiri kutokana na maandalizi waliyofanya kucheza aprili 10 mwaka huu na sio kesho.
Kizuguto alisema licha ya kuwepo changamoto kama hizo, wao wanaheshimu kila mchezo huku wakihitaji ushindi na kuweza kumaliza ligi msimu huu wakiwa mabingwa wa taji hilo.
“Tumejipanga kushindana katika uwanja wa nyumbani dhidi ya timu ngumu ya JKT Oljoro, tunajua fika kuwa maafande hawa ni wagumu sana, lakini tumefanya maandalizi makubwa sana kuhakikisha tunapata matokeo ya ushindi”. Alisema Baraka.
Akizungumzia afya za wachezaji wao, Kizuguto alisisitiza kuwa wachezaji wote wapo kambini wakiwa salama na wanaendelea na mazoezi ya mwisho mwisho kuwakabili Oljoro hapo kesho.
“Yanga haina majeruhi ambaye yupo hatarini kuukosa mchezo wa kesho, kilichobaki ni kusubiri muda ufike ili tukacheze mechi hiyo”. Alisema Kizuguto.
Pia afisa habari huyo aliwataka wapenzi na wanachama wa Yanga kufika kwa wingi uwanja wa taifa ili kuwapa nguvu wachezaji wao wenye lengo la kuwapatia zawadi ya ubingwa msimu huu.
Wakati Yanga wakijinasibu kuwa wako barabara, nao Oljoro wamejibu mapigo kuwa kesho ni kutafuta heshima mbele ya vinara wa ligi hiyo na wakongwe wa soka la Tanzania.
Kocha msaidizi wa klabu hiyo Riziki Shawa,  amesema kuwa wao wameshapanga makombora ya kuwamaliza Yanga wenye ngebe ya kutwaa ubingwa msimu huu.
“Kinachowabeba Yanga kwa sasa ni bahati tu, timu yao ni ya kawaida sana, sisi tumejipanga kuwaadabisha katika uwanja bora wa taifa mbele ya umati wa mashabiki wao”. Alijigamba Shawa.
Shawa alisema klabu hiyo tayari ipo jijini Dar es salaam tayari kwa kuwavaa wanajangwani hapo kesho.
Yanga kwa sasa wapo kileleni wakijikusanyia pointi 49 kibindoni, huku Azam fc wakiwa nyuma yao kwa pointi 46 lakini Azam wamecheza mechi moja zaidi.
Kama Yanga watashinda kesho wataweka pengo la pointi 6 huku wakisubiri mchezo wa jumapili kati ya mabingwa watetezi Simba dhidi ya wana lambalamba Azam fc mchezo utakaopigwa uwanja wa taifa.
 

3 comments:

Francis Kivuyo said...

JKT Oljoro,wawakilishi pekee wa A-town,ama ukipenda Genever ya Africa, nawatakia kila la heri,waadabisheni hao YANGA!

Francis Kivuyo said...

oljoro wakimbizeni yanga! hawana lolote.

Francis Kivuyo said...

good news, thanks!

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video