Thursday, April 11, 2013



 
Na Baraka Mpenja
Usaili wa wachezaji watakaoshiriki michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 12 na 14 manispaa ya Ilala inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mei mosi mwaka huu umepangwa kufanyika aprili 13 na 14 mwaka huu majira ya saa sita mchana katika uwanja wa karume jijini Dar es salaam.
Akizungumza na Mtandao huu mwenyeki wa chama cha soka la vijana wilaya ya Ilala (IDYOSA), Father Edwirn Mloka amesema usaili huo wenye lengo la kupata umri sahihi kwa timu shiriki utajumuisha timu 11 za wilayani hapo.
Mloka alisema jumamosi ya Aprili 13, usaili utafanyika kwa timu za Tabata Rangers, Home Team, Vumbua vipaji, New Team, Muheza Kids na Tabata Twiga.
Siku inayofauta aprili 14 timu za Kinota, Makoba, Sinepa Academy, Elimu Kids na Lili Boys zitafanyiwa usaili huo.
Mwenyekiti huyo wa IDYOSA, alisisitiza kuwa viongozi wa timu hizo wanatakiwa kufika bila kukosa na muda lazima uzingatiwe kama ulivyopangwa.
“Soka la vijana linatakiwa kuzingatia nidhamu, kuchelewa ni moja kati ya makosa ya utovu wa nidhamu, kama wachezaji watachelewa kufika kwa sababu ya uzembe wa viongozi, hakika watachukuliwa hatua za kinidhamu”. Alisema Mloka.
Mloka alisema soka la sasa linahitaji kuwezekeza kwa vijana wadogo, hivyo wilaya ya Ilala inataka kuwa mfano wa kuigwa kwa wilaya zote nchini Tanzania.
Kiongozi huyo mwenye hulka ya kuendesha soka la vijana, aliongeza kuwa lazima wadau wa soka, makampuni mbalimbali yakubali kuwekeza katika soka la vijana kwani ndio msingi wa taifa lolote.
“Mara nyingi tunahangaika kutafuta misaada wakati watu wenye uwezo wanajitokeza kudhamini timu za ligi kuu, lazima watambue kuwa msingi wa soka kwa sasa ni vijana wadogo ambao siku zote hufundishika kirahisi kuliko wakongwe”. Aliongeza Mloka.
Mbali na zoezi la usaili, Mloka alisema chama chake kimepata mwaliko wa kupelekea timu ya soka mkoani Tabora mwezi juni mwaka huu ili kudumisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu wa kuongoza soka la makinda kwa wilaya hizo mbili.
Mloka alisisitiza kuwa mashindano yanayoanza mwezi ujao yatasaidia kupata timu ya kusafiri mpaka kwa wanyamwezi wa Tabora, hivyo kila timu shiriki iwaandae vijana wake kushindana na kutoa wachezaji wa kwenda huko.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video