Sunday, April 14, 2013

simba na azam fc

Na Baraka Mpenja
Baada ya Prisons na Yanga kuunguruma katika michezo yao ya jana, leo kipute kingine cha kukata na shoka ni uwanja wa taifa ambapo wekundu wa msimbazi Simba `Taifa Kubwa` wakiwa ya kocha Mfaransa Patrick Liewig watakuwa kibaruani kupepetana na Azam fc maarufu kama wana Lambalamba wanaonolewa na kocha Mwiingereza Sterwart Jan Hall.
Mtanange huo umevuta hisia za mashabiki wa soka kutokana na kuibuka upinzani mkubwa baina ya timu hizo mbili.
Mechi ya mzunguko wa kwanza mwaka jana, Azam walipoteza mchezo baada ya kukubali kipondo cha mabao 3-2 wakati kipindi cha kwanza walikuwa wanaongoza 2-0, lakini kimbembe kiliwaangukia kipindi cha pili baada ya Mnyama kusawazisha yote na kutia kambani msumari wa ushindi.
Baada ya mechi ile baadhi ya wachezaji wa Azam walikalia kuti la moto kwa tuhumu za kula rushwa kutoka kwa Simba.
Wachezaji hao ni mabeki Aggrey Morris, Said Morad, na Erasto Nyoni, pia mlinda mlango namba moja kwa wakati ule  Deogratius Munish `Dida` alikumbwa na tuhuma hizo.
Azam waliwapeleka wachezaji hao TAKUKURU lakini hivi karibuni taasisi hiyo ilitangaza kuwa uchunguzi umeshindwa kubaini kama kweli walikula mlungula hivyo iliwaachia huru.
Sasa Azam wamewajumuisha nyota hao katika kikosi chao na kinachosubiriwa ni maamuzi ya kocha kuwapanga katika kipute cha leo ama la.
Kuelekea katika mchezo huo kila timu imesema maandalizi yamekamilika na kinachosubiriwa ni muda kufika ili shughuli ianze uwanjani.
Azam fc kupitia kwa Afisa habari wake Jafar Idd Maganga walisema maandalizi ya mtanange huo yamekamili, wachezaji wote wapo salama na wana morali kubwa ya kupata pointi tatu muhimu ili kuwasogelea Yanga waliopo kileleni kwa pointi 52 sasa baada ya jana kushinda dhidi ya Oljoro.
“Sisi kila mechi kwetu ni fainali, tunajiandaa kukabiliana na Simba ambao wameshapoteza ubingwa wao na sasa wanaiwinda nafasi ya pili, tunalifahamu hilo na ndio maana tumejipanga barabara kukabiliana nao leo”. Alisema Idd.
Idd aliongeza kuwa Simba wana timu nzuri ambayo inaweza kupata matokeo ya ushindi ingawa kuna baadhi ya watu wanawabeza.
“Wapinzani wetu wanawatumia vyema vijana wao, licha ya kutokuwa na matokeo mazuri mechi mbili zilizopita bado wanaweza kufanya lolote, lakini tuko kikosi kamili kwani wachezaji wote wapo salama kuumana na Mnyama”. Alijinasibu Idd.
Wakati Azam wakijigamba kutumia vyema mchezo huo, kwa upande wa Simba wamesema wamejiandaa vizuri kupambana na wapinzani wao ambao wana moto wa kushiriki michuano ya kimataifa.
Akizungumza na matandao huu kocha msaidizi wa Simba Jamhuri Kiwhelu Julio, alisema kwanza wanamshukuru mungu mwingi wa rehema kwani kikosi kipo salama kukabiliana wapinzani wao.
Julio alisisitiza kauli yake kwamba Mashabiki wa Simba wawe na subiri baada ya kupoteza taji lao msimu huu kwani Simba hii wanayoidharau wataipenda tu msimu ujao.
“Vijana tunaowatumia wanafanya vizuri sana na kama wataenedelea kujiamini watawabeba sana wana msimbazi. Azam ni wazuri lakini hatukati tamaa hata kidogo tutapambana nao kufa na kupona ili angalau tushike nafasi ya pili”. Alisema Julio.
Kocha huyo aliyejaaliwa kuwa na maneno mengi aliongeza kuwa mashabiki wa simba wajitokeze kwa wingi leo hii kuwashuhudiwa vijana wao wakifanya kazi nzuri ndani ya dimba murua la taifa maeneo ya Chang`ombe jijini Dar es salaam.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video