Na Baraka Mpenja
Wakata miwa wa kagera sugar
wanajiandaa na kibarua kigumu cha kuwakabili wapinzania wao wa kanda ya
ziwa Toto Africa kesho kutwa katika dimba lao la nyumbani, Kaitaba mjini
Bukoba.
Mzunguko wa kwanza Kagera sugar
waliwatungua Toto mabao 2-1 katika uwanja wa CCM Kirumba na sasa
wanakutana tena bukoba kuonshana shughuli pevu.
Kocha mkuu wa klabu ya Kagera
sugar, Abdallah Kibadeni “King Mputa” amesema leo hii asubuhi wameanza
mazoezi ya kujiandaa na mchezo huo.
“Tumepumzika kwa siku nyingi
lakini leo hii vijana wamefika uwanjani ili kuwekana sawa kabla ya
kuwavaa ndugu zetu Toto wenye nia ya kukwepa mkasi wa kushuka daraja”.
Alisema Kibadeni.
Kocha huyo aliyewahi Kutamba na
simba akicheza winga miaka ya sabini pia kuwa kocha wake, aliongeza kuwa
mchezo huo ni mgumu sana kutokana na ukweli kwamba wapinzania wao
wanausaka ushindi kwa nguvu zote, lakini vijana wake wanajengwa
kupambana kwa mbinu nyingi za kiufundi ili kuwadhibiti wana
kishamapanda.
Kibadeni alisema hesabu zake ni
kupata nafasi nzuri katika msimamo ili kupata angalau nafasi ya kucheza
michauno ya kimataifa hivyo mchezo wa keshokutwa ni lazima kushindi ili
kuongeza kasi yake zaidi.
“Tupo nafasi ya tatu kwa pointi
37, simba wanakuja nyuma yetu, najua wanapambana kweli , lakini sisi
tunajipanga kuhakikisha hatutoki pale tulipo labda tusonge mbele zaidi”.
Alisisitiza kibadeni.
Akizungumzia hali ya ligi hususani
dakika hizi za lala kwa buriani, Kibadeni alisema ligi kuu imekuwa
ngumu zaidi kwani kila timu inaonekana kujipanga zaidi ili kujiweka
mazingira mazuri.
“Hakika hadi dua za mashabiki kwa
sasa zinahusika sana, wana Kagera watuunge mkono ngwe hii ya lala
salama, kikubwa wasiliachie kampuni pekee kwani hata wao wanatakiwa
kutusaidia hata kwa kujitokeza kwa wingi uwanjani”. Alisema King
Kibadeni.
1 comments:
Imenibamba!
Post a Comment