BOSI wa muda Chelsea, Rafa Benitez, amesema Timu yake
ilistahili kupewa Penati Dakika za mwishoni jana walipofungwa Bao 2-1 na
Manchester City Uwanjani Wembley kwenye Mechi ya Nusu Fainali ya FA CUP.
Kipigo hicho kimewapokonya Chelsea FA CUP ambalo wao ndio
walikuwa Mabingwa watetezi.
Man City sasa wametinga Fainali na watacheza na Wigan
Athletic ambao Jumamosi waliwafunga Millwall Bao 2-0 katika Nusu Fainali
nyingine.
Lakini Benitez amelalamika kwa Refa Chris Foy kutotoa Penati
wakati Vincent Kompany wa Man City alipoonekana waziwazi akimvuta Jezi Fernando
Torres.
Benitez ametamka: “Sipendi kumyooshea kidole Mchezaji,
lakini ile ilikuwa Penati na ilitakiwa iwe Penati na Kadi Nyekundu. Ingebadilisha mchezo
na inabidi Marefa wajieleze!”
Mbali ya tukio hilo la Penati tukio jingine baya ambalo
halikuonwa na Refa Foy ni pale Segio Aguero wa Man City alipomrukia David Luiz
kwa miguu miwili, rafu ambayo ilistahili Kadi Nyekundu moja kwa moja.
Lakini Luiz amesema hana kinyongo kwa rafu hiyo kwani
kawaida Aguero si Mchezaji mchafu.
Benitez, ambae Timu yake Chelsea sasa ina nafasi moja tu
iliyobaki kutwaa Kikombe Msimu huu ambayo ni kupitia EUROPA LIGI ambako wako
Nusu Fainali na watacheza na Basel FC hapo Aprili 25, amesema mkazo wao sasa ni
kwenye BPL, Barclays Premier League, ambako nia yao ni kumaliza kwenye
0 comments:
Post a Comment