Sunday, April 14, 2013

Carlos Tevez na David Luiz
Carlos Tevez na David Luiz
Na Supersport.com
Mabingwa watetezi wa kombe la FA nchini England watakuwa kibaruani leo hii majira ya saa 12 jioni katika uwanja wa taifa wa Wembley kupepetana na mabingwa watetezi wa taji la ligi kuu soka nchini England, klabu ya Manchester city mchezo wa nusu fainali ya pili ya FA.
Miamba hiyo imeshindwa kupambana na mashetani wekundu kuwania taji la ligi kuu msimu huu ingawa Chelsea wamefika hatua ya nusu fainali ya ligi ya UROPA, lakini mchezo huu utakuwa muhimu kwao wote ili kumaliza msimu angalau na kikombe kimoja.
Mshindi wa mchezo wa leo utakumbana naWigan Athletic katika mtanange wa fainali baada ya klabu hiyo  kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu ya daraja la Championship, Millwall na kutinga hatua ya fainali.
Kocha wa muda wa Chelsea Rafael Benitez na wa City  Roberto Mancini wote kwa pamoja wanawania kutwaa kombe kwa mara ya pili wakifanya kazi nchini Uingereza.
Mwishoni mwa mwezi februari mwaka huu timu hizo zilikutana katika dimba la Etihad katika mchezo wa ligi kuu na kushuhudia City wakiwabamiza wapinzani wao mabao 2-0,  lakini Benetez amesema amejifunza kwa kiasi kikubwa.
“Tunajua itakuwa mechi ngumu, lakini ni nusu fainali yenye ushindani mkubwa”. Alisema Mhispania huyo aliyetwaa ubingwa wa kombe hilo mwaka 2006 akiwa na wekundu wa Anfield, klabu ya Liverpool.
Benetez aliongeza kuwa City ni timu nzuri, ina kikosi bora na kocha mzuri mwenye uzoefu mkubwa,  lakini watajituma zaidi endapo wanataka kuibuka kidedea katika kipute hicho.
City wanaingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu nzuri ya kuwafumua watani zao wa jadi Manchester United mabao 2-1 katika uwanja wa Old Traford jumatatu ya wiki hii mchezo wa ligi kuu soka Uingereza.
Mancini amekuwa na presha kubwa baada ya kuweka rehani ubingwa wake mbele ya united, lakini bado ana nafasi ya kujikusanyia kombe la tatu ndani ya miaka mitatu.
Kocha huyo aliondoa ukame wa City kutotwaa ubingwa wa kombe la FA kwa miaka 35 baada ya kuiongoza klabu yake kunyakua ubingwa mwaka 2011 akiwafunga Stoke city mchezo wa fainali.
Mancini alisema, “nadhani kucheza Wembley ni bonge la mechi kwa mashabiki wote wa soka hivyo ni nafasi muhimu kushuhudia mechi hiyo ya nusu fainali”.
Kocha huyo aliongeza kuwa kila kombe ni muhimu kwa timu zote, lakini kwa upande wao ni muhimu zaidi kwani wana nafasi ya kutinga fainali na kubeba kombe hilo kwa mara ya pili ndani ya miaka mitatu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video