………………………………………..
Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa
Nchini TPBC) imetangaza kuanza kufanya uchaguzi katika ngazi ya mikoa
kuanzia tarehe 20 February 2013.
Katika chaguzi hizo,
mikoa itafanya chaguzi zake kuwachagua viongozi wake katika nafasi za
Kamishna wa mkoa, Katibu, Katibu Msaidizi, Mweka Hazina, Mweka Hazina
Msaidizi pamoja na wajumbe 10 wa Kamati ya Utendaji ya Mkoa.
Mikoa ambayo itafanya chaguzi ni
pamoja na Kilimanjaro, Arusha, Mbeya, Dar-Es-Salaam, Morogoro, Tanga,
Pwani, Mwanza, Mara na Bukoba.
Baada ya chaguzi za mikoa TPBC
itafanya uchaguzi mkuu katika ngazi ya Taifa mwishoni mwa mwezi wa tatu
(Machi) 2013. Wadau wa ngumi wanahimizwa kujitokeza kwa wingi ili waweze
kushiriki katika chaguzi hizi.
Rais wa TPBC Onesmo Ngowi
ameshatangaza kuwa hatagombea tena uongozi katika Kamisheni na kuwataka
Watanzania wanaopenda mchezo wa ngumi kujitokeza ili waweze kuiongoza
Kamisheni.
0 comments:
Post a Comment