
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kama ishara ya uzinduzi
wa Jengo la Bohari Kuu ya Dawa,Maruhubi Nje ya Mji wa Zanzibar jana
ikiwa ni shamra shamra za kilele cha miaka 49 ya Mapinduzi Matukufu
ya zanzibar,(kulia) Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Alfonso
Lenhardt.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akikata utepe kama ishara ya uzinduzi
wa Jengo la Bohari Kuu ya Dawa,huko Maruhubi Nje ya Mji wa Zanzibar
jana ikiwa ni shamra shamra za kilele cha miaka 49 ya Mapinduzi
Matukufu ya zanzibar,(kulia) ni Naibu waziri wa Afya Sira Ubwa Mamboya
na Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Alfonso Lenhardt.[Picha na
Ramadhan Othman,Ikulu.]

Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa
Bohari Kuu,Said Mohamed,(kulia) alipotembela sehemu ya kuhifadhia
Dawa,baada ua uzinduzi wa Jengo la Bohari Kuu ya Dawa huko Maruhubi
Nje ya Mji wa Zanzibar,ikiwa ni shamra shamra za kilele cha miaka 49
ya Mapinduzi Matukufu ya zanzibar,(wa tatu kushoto) Balozi wa
Marekani Nchini Tanzania Alfonso Lenhardt.[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]

Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa tatu Kulia)pamoja na Viongozi
wengine akiwemo Balozi wa Marekani Nchini Alfonso
Lenhardt.wakiangalia namna ya uchukuwaji dawa kwa kutumia mashine
maalum na kutoa nje ya Bohari kuu ya Dawa,baada ya ufunguzi rasmi jana
huko Maruhubi Nje ya mji wa Zanzibar,ikiwa ni shamra shamra za kilele
cha miaka 49 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzíbar
………………………………………………
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
amesema uzinduzi wa Bohari kuu ya Dawa utaiwezesha Serikali ya Mapinduzi
Zanzíbar kupanga bajeti yake vyema ya dawa na kusaidia utoaji wa huduma
za afya kwa ubora wa hali ya juu.
Rais
Shein ameyasema hayo katika hafla ya uzinduzi wa Bohari Kuu ya Dawa
iliyopo Maruhubi mjini Zanzibar ikiwa ni mwendelezo wa shamra shamra za
kutimiza miaka 49 ya Mapinduzi Zanzibar.
Amesema
Bohari hiyo ya kisasa ni matunda ya kujivunia ya Mapinduzi ya Zanzibar
ambayo kwa hakika italeta tija katika upatikanaji wa dawa na uimarisha
wa afya za wananchi.
Dkt.
Shein ameelezea matumaini yake kwa sekta ya afya kupitia Bohari hiyo na
kwamba anaamini baada ya miaka mitatu Zanzibar itakuwa haipeleki tena
Wagonjwa nje ya nchi kwa matibabu.
Aidha
Dkt. Shein amewataka watumishi wa Serikali kubadilika kiutendaji
kulingana na kasi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wa Bohari
hiyo kuitunza vyema ili iendelee kutoa huduma kama inavyotakiwa.
Kwa
upande wake Naibu Waziri wa Afya Sira Ubwa amesema Bohari hiyo
itaboresha utoaji wa huduma kwa uhakika kutokana na ubora wa vifaa na
mitambo ya kisasa ambapo wataalamu wataweza kubaini mahitaji ya Dawa
zinazohitajika katika kila Hospitali za Unguja na Pemba.
Kwa
upende wao Mabalozi wa Marekani na Denmark wameelezea kufurahishwa kwao
na juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha afya
ya Wananchi hasa katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Malaria na Ukimwi.
Aidha
wameahidi kuendelea kutoa mashirikiano kwa Serikali hasa katika huduma
za Afya kwa Mama na Watoto, Elimu,Mapambano dhidi ya magonjwa ya
maambukizi pamoja na uzazi wa mpango.
Bohari
hiyo iliyojengwa na Serikali ya Mapinduzi kwa msaada wa Shirika la
USAID na NIDA inaelezewa kuwa ya tatu duniani katika viwango vya ubora
ambapo jumla ya Dolla za Kimarekani Milion 1.2 zimetumika kukamilisha
ujenzi wake.
0 comments:
Post a Comment