Friday, June 30, 2017


“Sijawahi kukata tamaa kwenye maisha yangu, kila siku napambana kufika sehemu ambayo naamini nastahili niwe na ninaamini ipo siku nitafika huko,” anasema Abasarim Chidiebere ambaye amesaini mkataba wa miaka miwili na klabu ya Caps United ya Zimbabwe.

“Tangu nilipokuja Tanzania, sijawahi kurudi nyumbani kwetu Nigeria, yote ni kwa sababu bado naamini natakiwa kupambana zaidi ili kufikia malengo yangu.”
Chidiebere amesema, sio kama hapendi kwenda kwao lakini haendi nyumbani kwa sababu bado malengo yake hayajatimia ya kucheza soka la kulipwa kwenye timu ya ndoto yake ambayo itampa mafanikio ya kutwaa mataji na kujulikana Afrika nzima pamoja na duniani.
“Akilini kwangu ninajua kwamba siku moja nitaenda nyumbani Nigeria na kukutana na familia yangu, nimekuwa nikiwasiliana nao mara kwa mara kuwajulia hali na kuwaambia maendeleo yangu nikiwa huku nchi za ugenini.”
Nimemuuliza Chid ilikuwaje akapata timu Zimbabwe wakati akiwa hapa nyumbani hakuna klabu iliyoonesha kumuhitaji kwa ajili ya msimu ujao mara baada ya mkataba wake na Stand kumalizika.
“Nina agent wangu ambaye ndio anashughulikia mambo yangu mengi ya nje ya uwanja, alinitafutia timu nikaalikwa Zimbabwe na klabu ya Caps United kwa ajili ya kufanya majaribio. Nilipofika hapa nilifanya kila ninachoweza ili nipate nafasi ya kupewa mkataba na hatimaye imekuwa hivyo.”
“Mimi niliamua kuanzia Tanzania kucheza soka langu kimataifa na ninashukuru kupitia Tanzania nimeweza kuvuka na kusogea mbele kidogo, Tanzania bado ni nyumbani kwangu kwa sababu nimepata mke hapa na mtoto pia.”
“Chidiebere amesema kwa sasa yupo pekeake Zimbabwe anaendea kukamilisha baadhi ya taratibu na kila kitu kikiwa sawa atakuja kuichukua familia yake (mke wake Tabitha na mtoto wao Chinonso).”

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video