Thursday, December 22, 2016

Ligi kuu soka Tanzania Bara inaendelea kesho kwa mechi moja kuchezwa Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salaam kati ya African Lyon dhidi ya mabingwa watetezi Yanga.
African Lyon wataingia katika mchezo wa kesho wakiwa na kumbukumbu ya kutoka suluhu na Azam FC kwenye mechi ya Jumapili iliyopita Uwanja wa Uhuru, wakati Yanga wao walishinda mabao matatu kwa bila dhidi ya JKT Ruvu.

Ugumu wa mechi ya African Lyon na Yanga unatokana na mazingira ya timu zote mbili kwenye msimamo wa Ligi kuu ambapo Yanga wapo katika mbio za Ubingwa wakizidiwa pointi mbili na vinara Simba wanaoongoza kwa pointi 38 baada ya timu zote kushuka dimbani mara 16.

African Lyon wao wapo kwenye harakati za kukwepa kushuka daraja wakiwa nafasi ya 12 kwenye msimamo wa VPL wakijikusanyia kibindoni pointi 18 katika mechi 16 walizoshuka dimbani .

Hata hivyo Yanga wamekuwa na rekodi nzuri dhidi ya African Lyon kwani hata mechi ya mzunguko wa kwanza iliyochezwa Agosti 28 mwaka huu, Yanga waliibuka na ushindi wa mabao matatu kwa bila.

Mabao ya Yanga kwenye mchezo huo yalifungwa na Deus Kaseke, Simon Msuva na Juma Mahadhi.
Mechi nyingine sita za VPL zitachezwa Jumamosi hii kwa Mbeya City, Wanakoma Kumwanya kuwa wenyeji wa Toto African Wanakisha Mapanda katika Uwanja wa Sokoine, Jijini Mbeya.

Wana Supankurukumbi Kagera Sugar watakuwa dimbani kwao Kaitaba kuwakabili Stand United, Chama la Wana.

Huko Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara, Ndanda FC, watapepetana na Kagera Sugar, huku Nyasi bandia za Uwanja wa Uhuru zikiwaka moto kwa vinara Simba kukabiliana na Maafande wa JKT Ruvu Stars.

Majimaji Wanalizombe watakuwa wenyeji wa Azam FC uwanja wa Majimaji mkoani Ruvuma, wakati Matajiri wa madini ya Almasi, Mwadui FC watawaalika Mbao FC kwenye uwanja wa Mwadui, mkoani Shinyanga.


Mzunguko huo wa 17 wa VPL utamalizika Boxing day Jumatatu ya Juma lijalo kwa Ruvu Shooting kucheza na Tanzania Prisons Uwanja wa Mabatini Pwani.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video