Thursday, December 22, 2016

Klabu ya Chapecoense ya Brazil ambayo hivi karibuni ilipoteza takribani kikosi kizima kutokana na ajali ya ndege iliyotokea karibu na mji wa Medellin nchini Colombia, rasmi imekabidhiwa kikombe cha ubingwa wa Sudamericana.
Itakumbukwa kikosi hicho kilikuwa kikielekea nchini Colombia kwaajili ya mchezo wake wa mwisho wa fainali ya klabu bingwa ukanda wa America ya Kusini dhidi ya wenyeji Atletico Nacional kabla ya kukumbwa na msiba huo mzito.

Wapinzani wao kwa kushirikiana na waandaji waliamua kuwakabidhi ubingwa huo kama sehemu ya kuomboleza kile kilichowakuta na hatimaye wapewa ubingwa wao wakati wa droo ya pangazi wa michuano ya msimu ujao.

Chapecoense imepangwa kundi moja na Club Nacional ya Uruguay, Zulia ya Venezuela na Lanus ya Argentina.


Kikosi hicho kitashuka kwa mara ya kwanza dimbani tangu kutokea kwa ajali hiyo Januari 29 mwakani ikiwa ni siku nne tu baada ya Brazil kucheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Colombia mjini Rio, lengo la mchezo huo ni kukusanya fedha kwaajili ya kuichangia Chapecoense.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video