Thursday, December 22, 2016

Shirikisho la Soka nchini TFF limeanza kufikiria kubadili tarehe ya mchezo wa mzunguko wa pili wa ligi kuu soka Tanzania Bara VPL kati ya watani wa jadi Simba na Yanga maarufu kama Dabi ya Kariakoo ambao umepangwa kufanyika Februari 18 mwakani.
Hatua hii imetokana na siku hiyo kuingiliana na mechi ya marudiano ya raundi ya awali ya ligi ya mabingwa barani Afrika ambayo wawakilishi wa Tanzania Yanga watachuana ugenini na Ngaya FC ya Comoro.

Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, JONAS KIWIA amethibitisha kwamba kutokana na muungiliano wa ratiba hiyo ya CAF, hawana jinsi zaidi ya kupangua mchezo huo wa VPL.

Kwa mujibu wa Droo ya CAF ya Ligi ya mabingwa Afrika iliyotolewa jana, Yanga watacheza mechi ya kwanza ya raundi ya awali kati ya Februari 10, 11 au 12 Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam ambapo wameingia mkataba na serikali juu ya kutumia uwanja huo kwenye mashindano ya CAF,  wakati mechi ya marudiano inatarajiwa kuwa kati ya Februari 17, 18 au 19 nchini Comoro.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video