Thursday, December 22, 2016


Chama cha soka cha Afrika kusini (SAFA) kimemtimua Ephraim 'Shakes' Mashaba aliyekuwa akiinoa Bafana Bafana na kuahidi kumchukulia hatua za kinidhamu kocha huyo mwenye miaka 66.
Kibarua cha Shakes Mashaba kilionekana kipo mashakani baada ya kuwatolea mbovu waajiri wake wakati kikosi chake kilipopata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Senegal katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali zijazo za kombe la dunia mwezi uliopita.

Aliadhibiwa kwa kuodolewa kwenye orodha ya msafara wa timu ya Taifa ya Afrika Kusini uliokwenda mjini Maputo na kuanzia hapo alikuwa na wakati mgumu wa kutetea ugali wake.

Mashaba aliiongoza Bafana Bafana katika AFCON ya mwaka 2015 lakini mafanikio hayo yaliingiwa na shubiri baada ya kushindwa kuipeleka Gabon kwenye za kombe la mataifa ya Afrika mwezi Januari mwakani.

SAFA imetoa tamko rasmi la kuachana na Kocha huyo ambae amepelekwa katika kamati ya nidhamu iliyosikiliza shauri lake kwa muda wa siku tano mwezi huu lililoongozwa na mtaalamu huru wa masuala ya sheria anaefanya kazi za uwakili kwenye mahakama kuu.

Baada ya kuhitimisha shauri hiyo Mwenyekiti wa kikao alitangaza kumtia hatiani kocha huyo kwa mambo makubwa matatu.

Jambo la Kwanza na la pili, amekiuka ufanisi wa kazi yake kama mkufunzi mwenye taaluma na jambo la tatu amevunja taratibu za mawasiliano za SAFA.


Mtendaji mkuu wa Chama hicho Dennis Mumble amesema chama cha chake kitaanza mchakato wa kumtafuta mrithi wa Mashaba hivi karibuni na moja ya kigezo muhimu, kocha huyo anapaswa kuwa na ufahamu na soka la barani Afrika.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video