Heshima ya mshambuliaji, Mbwana Samatta inazidi kupanda katika kikosi chake cha KRC Genk ya Ubelgiji na sasa achukuliwa kama moja ya wachezaji muhimu zaidi klabu hapo.
Hiyo inatokana na Samatta kuwa miongoni mwa wafungaji mahiri kwenye ligi ya Ubelgiji, Pro League, na tayari ana mabao manne.
Wakati anasajiliwa na Genk akitokea TP Mazembe ya DR Congo, haikuwa rahisi kuona Samatta akiwekwa kwenye matangazo muhimu ya Genk (Poster).
Kutumika kwenye matangazo ni sehemu ya kuonesha una mvuto au unakubalika. Jambo ambalo ni bora kwa Samatta na anachotakiwa ni kuongeza tu juhudi.
Ikumbukwe kwamba Genk alifuzu kucheza hatua ya makundi ya Uefa Europa League msimu huu na walipangwa kundi F na timu kubwa kama Athletic Club ya Hispania (kama inavyoonekana chini na ratiba ya mechi zenyewe).
Tayari Genk wameanza kuzitangaza mechi zao kwa kutumia wachezaji wao muhimu akiwemo Mbwana Samatta (Tazama picha juu).
0 comments:
Post a Comment