Golikipa mkongwe nchini, Ivo Philip Mapunda amesema yuko
tayari kusaini mkataba na klabu yake ya Simba, lakini amekuwa haelewi kama kweli wekundu hao wa Msimbazi wanamhitaji tena.
Ivo amekaririwa na Salehjembe akisema kamwe hajakimbia kama ambavyo imekuwa ikielezwa.
“Nimekimbia vipi, mara ya
mwisho niliondoka kambini Lushoto baada ya kuumia. Collins (Kaimu Katibu Mkuu)
alinieleza atanipa mkataba.
“Nimekuwa nikisubiri na hata
niliwasiliana na kocha pamoja na Collins, bado inaonekana kuna sintofahamu.
“Si kweli nimekimbia, nipo
tayari lakini vizuri nao wakaonyesha wana nia kweli ya kufanya kazi na mimi,”
alisema Ivo.
Kuhusiana na hilo, Rais wa
Simba, Evans Aveva amesema wanachosubiri na Ivo ni kusaini mkataba tu.
“Kuhusu Ivo tulishamalizana,
tunachosubiri kusaini naye mkataba. Hatukumpata kumalizana naye lakini taarifa
zinaeleza yuko jijini Dar.
“Hivyo itakuwa lahisi kumpata
na kumalizana naye. Baada ya
kusaini mkataba, basi tutawapa taarifa,” alisema Aveva.
Ivo aliumia wakati akiwa
Lushoto akalazimika kuondoka kambini kwenye kupata matibabu. Makubaliano yake
na Simba ni kuongeza mkataba wa mwaka mmoja, jambo ambalo linaelezwa
litafanyika kati ya leo, kesho na keshokutwa.


0 comments:
Post a Comment