Raheem Sterling alipoteza nafasi nzuri ya kufunga dhidi ya West Brom,lakini bado ndiye alikuwa mchezaji bora wa mechi ambaye aliwavutia mashabiki wa Manchester City.
Kufuatia timu yake kuanza ligi ya England kwa ushindi wa 3-0 ugenini, Sterling aliyesajiliwa kwa paundi milioni 49 kutokea Livrpool, alienda eneo la mashabiki ili kuwapatia jezi yake aliyotumia kwenye mechi hiyo.
Sterling aliwapuuza walinzi wa uwajani na kuwachagua mashabiki wawili ili awapatie jezi.
Mashabiki hao walionekana kuwa na furaha kubwa zaidi na
Sterling akaelekea moja kwa moja katika vyumba vya kubadilishia nguo ambako walishangilia pia ushindi huo mnono.

Nyota wa zamani wa Liverpool akiruka uzio wa matangazo ya uwanjani kwenda kuwapatia jezi mashabiki

Mashabiki wa Manchester City wakimtazama kwa ukaribu Sterling
Kocha wa Man City, Manuel Pellegrini ana matumaini kwamba Sterling ataendelea kuonesha kiwango kikubwa kwenye mechi inayofuata dhidi ya Chelsea ambayo itapigwa Etihad.
Mchile huyo alisema: "Sijakatishwa tamaa na nafasi aliyopoteza kwasababu Raheem alicheza vizuri ndani ya dakika 70".
"Sio rahisi kucheza mfumo mpya na wachezaji wapya, alifanya kazi nzuri na alipata nafasi nzuri"
"Kama ataendelea kucheza hivi, nina uhakika atakuwa aina ya mchezaji tuliyemnunua"

Wawili hawa wana bahati sana.

0 comments:
Post a Comment