Saturday, September 21, 2013

JWTZ
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI



Simu:  +255-22-2112035/40
          S.L.P.  9223
Nukushi:  +255-2122617/2120486
Barua Pepe:  [email protected]
       Dar es Salaam
Septemba 19,2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Julai 29, 2013 aliagiza kufanyika kwa opereheni maalum ya kuondoa uhalifu katika mikoa ya Kagera, Kigoma na Geita mbao kwa kiasi kikubwa umechangiwa na kuwepo kwa wahamiaji haramu kutoka nchi jirani.
Operesheni Kimbunga inayoongozwa na Brigedia Jenerali Mathew Sukambi imeanza rasmi Septemba 6, 2013 baada ya kutoa muda wawiki mbili kwa wahamiaji wanaoishi nchini bila kufuata sheria kuondoka kwa hiari yao au kuhalalisha ukaazi wao nchini.
Wakati Operesheni hii ikifikia katika Wiki yake ya Pili, Serikali kupitia kiongozi wa Operesheni Brigedia Jenerali Mathew Sukambi inawapongeza watendaji wote wa operesheni hii kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa unyenyekevu na kiuzalendo kuhakikisha kuwa zoezi la kuondoa uhalifu na kukamata wahamiaji haramu linafanyika kwa nidhamu ya hali ya juu na mafanikio.
Aidha, kumekuwepo na tuhuma mbali mbali zinazotolewa kupitia Vyombo vya Habari ambazo hazina ukweli.
Tuhuma za rushwa dhidi ya watendaji wa Operesheni Kimbunga
Operesheni Kimbunga inahusisha watendaji kutoka vyombo mbali mbali nchini vikiwemo Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Idara ya Uhamiaji, Jeshi la Polisi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa (TAKUKURU), Idara ya Usalama wa Taifa, Idara ya wanyamapori na taasisi nyingine za serikali.
Mazingira ya kazi ya kuwakamata wahamiaji haramu na kuwahoji ili kuthibitisha uraia wao  ni ya wazi hayawezi kuruhusu watendaji kuweza kupokea rushwa kama ilivyoripotiwa na Gazeti moja hapa nchini kwani kwa kufanya hivyo ni ukiukwaji wa sheria.
Hata hivyo, wananchi wanapaswa kufahamu kuwa iwapo kuna mtendaji wa operesheni hii ameomba na kupokea rushwa wanakiuka sheria, hivyo ni vyema kama kuna mtu mwenye ushahidi wowote atoe taarifa kwenye ofisi za TAKUKURU zilizopo mikoani na Wilaya zote nchini.
Zoezi la Operesheni Kimbunga halilengi kunyanyasa wazee, watoto na wanawake wasio Raia walioolewa na Watanzania
Operesheni Kimbunga haikulenga kuwanyanyasa Wazee, Wanawake walioolewa na watoto wao wadogo wanaoishi nchini bila kufuata Sheria ya uhamiaji.
 Kuna waliokuwa Wakimbizi 36,000 kutoka nchi ya Rwanda walioingia nchini miaka ya 1959 hadi 1961 waliokuwa wakiishi katika mkoa wa Kagera katika maeneo ya Kimuli, Nkwenda, Mwase na maeneo mengine ambao walipewa uraia wa Tanzania kwa tajinisi mwaka 1983 isipokuwa watoto wao kwa kuwa wazazi wao hawakuwaombea uraia huo.  Raia hao 36,000 waliopewa uraia wa tajinisi hawakuguswa na operesheni hii kwani ni watanzania isipokuwa watoto wao ambao hawakuombewa uraia na wanaishi nchini bila hadhi yeyote ya kiuhamiaji.
Pia kuna raia wa kigeni waliokuwa wanaishi bila kufuata sheria za uhamiaji na Uraia ambao zamani walikuwa wakimbizi lakini hadhi ya ukimbizi iliondolewa baada ya nchi zao kuwa salama na kutakiwa kurudi.
Hata hivyo, kama mheshimiwa Rais, Jakaya Mrisho Kikwete alivyoagiza kuwa zoezi lifanyike likiwa na sura ya kibinaadam pale inapobidi, raia hao wa kigeni waliokuwa wanaishi nchini bila kufuata sheria hususan wazee wameruhusiwa kubaki na kusaidiwa kufuata taratibu ili kuhalalisha ukaazi wao.
Aidha, ieleweke kuwa kuzaliwa Tanzania pekee  hakumpi mtu haki ya kuwa Raia moja kwa moja mpaka taratibu nyingine zifuatwe.  Kuna watoto walizaliwa Tanzania na Raia wa nchi za nje waliokuwa wanaishi nchini kabla ya kupatiwa uraia. Hao hawawezi kuwa raia moja kwa moja mpaka taratibu za kisheria zifuatwe. 
Aidha, Operesheni Kimbunga haikulenga kuvunja ndoa na kusambaratisha familia.  Lengo ni kuondoa wahamiaji haramu.
Wanawake walioolewa na Watanzania wametakiwa kujiorodhesha ili kupatiwa utaratibu wa ukaaji wao.  Wanaume walifunga ndoa na Watanzania wanatakiwa kurudi katika nchi zao na wake na watoto wao na kwa wanaotaka kuishi nchini wanatakiwa kuomba vibali vya kuishi kwa kufuata sheria na taratibu za uhamiaji.
Taarifa hii imetolewa na Zamaradi Kawawa, Kiongozi wa Timu ya Habari na Mawasiliano ya Operesheni Kimbunga, Septemba 20,2013, Biharamulo, Kagera. Kwa maelezo zaidi Email: [email protected].

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video