Mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara Yanga SC jana walishindwa kufurukuta mbele ya wababe wa ligi ya Kenya timu ya Gor Mahia baada kukubali kichapo cha goli 2-1 kwenye mchezo wa ufunguzi wa michuano ya Kagame Cup uliopigwa jana jioni kwenye uwanja wa Taifa.
Yanga walipata goli lao mapema dakika ya nne kipindi cha kwanza mfungaji akiwa ni Donald Ngoma lakini dakika ya 16 Haruna Shakava aliifungia Gor Mahia goli la kusawazisha na Michael Olunga akafunga goli la pili na la ushindi kwa upande wa Gor Mahia dakika ya 45 kipindi cha pili.
Haya ni matukio muhimu ambayo yalijiri uwanja wa Taifa kabla wakati na baada ya mchezo huo wa ufunguzi.
Waziri mkuu wa zamani wa iliyokuwa serikali ya umoja wa kitaifa ya Kenya Raila Odinga (katikati) aipunga mkono kwa mashabiki waliokuwepo uwanjani kushuhudia pambano la Yanga dhidi ya Gor Mahia
Mashabiki wa Yanga wakiwa hawana matumaini bada ya timu yao kufungwa goli la pili na timu ya Gor Mahia kwenye mchezo wa ufunguzi uwanja wa Taifa
Mshambuliaji mpya wa Yanga Malimi Busungu (kushoto) na golikipa namba mbili wa Yanga Deogratius Munishi ‘Dida’ wakifauatilia kwa makini mchezo wa jana
0 comments:
Post a Comment