Hizi ndizo tuzo zilizokuwa zinagombewa kabla hazijaanza kukabidhiwa kwa wahusika jana
BAADA ya minong’ono kuzuka juu ya watu waliopewa tuzo jana
hususani kocha bora na golikipa bora, Afisa mtendaji mkuu wa bodi ya ligi
(TPLB), Boniface Wambura amefafanua namna walivyopata washindi.
Mbwana Makata (Prisons) ameibuka kocha bora wa VPL baada ya
kuwashinda Hans van der Pluijm (Yanga) na Goran Kopunovic (Simba).
Shaban Hassan Kado naye ameibuka kipa bora akiwabwaga Said
Mohamed (Mtibwa Sugar) na Mohamed Yusuph (Prisons).
Wambura amesema mchakato wa kuwapata washinda ulianza wakati
ligi inaanza na katika kila uwanja unaochezewa mechi za ligi kuu kuna wataalamu
wanaochunguza mwenendo wa wahusika.
“TFF na bodi ya ligi tuna watu wa ufundi ambao wapo viwanja
vyote ambavyo mechi za ligi kuu ya Vodacom huchezwa. Kuna vigezo ambavyo
wataalamu hawa wanavyo katika kuchagua wachezaji, makocha, timu, golikipa bora
na mwamuzi bora. Vyote vinaangaliwa kwa kuzingatia vigezo ambavyo vipo”.
Amesema Wambura na kuongeza: “Lakini katika vigezo vyote, kuna kigezo ambacho
kipo katika vipengele vyote ambacho ni nidhamu ndani na nje ya uwanja, huu ni
mchezo wa kiungwana ‘Fair Play’ , lazima tufike mahala tutambue kuwa nidhamu
ndio kitu muhimu katika kufanikisha mpira wa miguu na michezo mingine kwa
ujumla”.
0 comments:
Post a Comment