Friday, June 12, 2015


Kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza maarufu kama ‘Simba watatu’ kiko katika maandalizi yake ya mwisho kuikabili timu ya taifa ya Slovenia katika mchezo wa kufuzu fainali za mataifa ya Ulaya Euro 2016, huku mshambuliaji nyota na nahodha wa timu hiyo Wayne Rooney akikaribia kuvunja rekodi ya ufungaji bora wa timu hiyo.

Katika mchezo huo utakao fanyika siku ya jumapili, Uingereza wanaongoza kundi wakiwa na pointi 15 katika michezo 5 waliyocheza kwa maana ya kushinda michezo yao yote ya awali, hawana majeruhi na wanatarajia kushinda katika mchezo huo kujiongezea nafasi ya kufuzu mapema iwezekanavyo.

Lakini kuelekea mchezo huo, mshambuliaji na nahodha wa timu hiyo Wayne Rooney ‘Wazza’ ndio stori kubwa kutokana na ukweli kwamba amebakiza magoli mawili tu, kuifikia rekodi ya ufungaji bora wa muda wote wa timu ya taifa ya nchi hiyo inayoshikiliwa na mkongwe Bob Chalton.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 29 hivi sasa, ameifungia Uingereza magoli 47 hadi sasa, huku Bob Chalton akiwa amefunga magoli 49.

Rooney na Bob Chalton wamejikuta katika hali hiyo hata katika ngazi ya klabu ambapo pia Chalton ndiye mfungaji bora wa klabu ya Manchester United huku Wayne Rooney ‘Shreak’ akiikaribia kwa ukaribu rekodi hiyo.


Kuna uwezekano mkubwa sana kwa Rooney kuzivunja rekodi hizo zote mbili kutokana na ukweli kwamba bado ana miaka kadhaa mbele ya kufanya vizuri katika klabu na taifa.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video